Tafuta

Maandamano na vurugu nchini Iran. Maandamano na vurugu nchini Iran. 

Papa Leo XIV,amani kwa ajili ya Ira,Syria&Ukraine:mazungumzo na uvumilivu

Mwishoni mwa sala ya Malaika wa Bwana,Dominika Januari 11,Papa Leo XIV alielekeza mawazo yake kwa Iran,eneo la maandamano na ukandamizaji na vurugu na kufanya Mazungumzo na amani kwa uvumilivu nchini Iran na Syria ambapo mapigano kati ya jeshi la serikali na wanamgambo wa Kikurdi yanaendelea:Fuateni manufaa ya jamii nzima.Alitoa wito wa amani nchini Ukraine,gizani na baridi kutokana na mashambulizi makubwa ya Urusi.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana, akiwageukia waamini na mahujaji waliokusanyika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, Dominika tarehe 11 Januari 2026 ikiwa ni Sherehe za Ubatizo wa Bwana Wetu Yesu, Baba Mtakatifu alisema: “Kaka na dada wapendwa, kama nilivyokwisha sema, asubuhi ya leo, kulingana na desturi ya Siku kuu ya Ubatizo wa Yesu, niliwabatiza watoto wachanga kadhaa, watoto wa wafanyakazi wa Makao Matakatifu.”

Baraka kwa watoto wote

Papa Leo kuhusu watoto aliendelea kusema: “Na sasa ningependa kuwapatia baraka zangu watoto wote waliopokea au watakaopokea Ubatizo katika siku hizi, huku Roma na ulimwenguni kote, nikiwakabidhi kwa ulinzi wa Mama wa Bikira Maria.” Papa Leo aliendelea kusema “Ninawaombea hasa watoto waliozaliwa katika hali ngumu zaidi, katika afya na kutokana na hatari za nje. Neema ya Ubatizo, inayowaunganisha na Fumbo la Pasaka la Kristo, ifanye kazi kwa ufanisi ndani yao na katika familia zao.”

Mawazo kwa Mashariki ya Kati: Iran ina Syria

Papa Leo XIV aidha alielekea nchi ambazo zimegubikwa ma vurugu na kusema: “Mawazo yangu yanageukia kile kinachotokea siku hizi Mashariki ya Kati, hasa Iran na Syria, ambapo mvutano unaoendelea unasababisha vifo vya watu wengi. Natumaini na kuomba kwamba mazungumzo na amani vitaendelezwa kwa uvumilivu, ili kutafuta manufaa ya jamii kwa ujumla.” Papa alikumbusha Nchi ya Ulaya Mashariki kwamba, “Nchini Ukraine, mashambulizi mapya, hasa makubwa, yanayolenga miundombinu ya nishati, yanaathiri vibaya raia, huku hali ya hewa ya baridi ikizidi kuwa mbaya. Ninawaombea wale wanaoteseka na kufufua wito wangu wa kukomesha vurugu na kuimarishwa kwa juhudi za kufikia amani.”


Salamu kwa mahujaji

“Na sasa ninawasalimu wote, Warumi na mahujaji mliopo leo katika Uwanja wa Mtakatifu Petro,” kwa njia hiyo Papa aliongoza kusema kwa lugha ya kiingereza na kihispania (thank you, muchas gracias!)”asanteni, shukrani nyingi! Kwa namna ya pekee, ninawasalimu kikundi kutoka Shule ya "Everest" ya Madrid na chama cha "Bambini Fratelli" cha Guadalajara, Mexico: Dejemos que los niños sueñen” yaani "Tuwaache watoto waote ndoto."Ninawatakia nyote Dominika njema!

Kabla ya sala na baada

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

11 Januari 2026, 14:07

Sala ya Malaika wa Bwana ni sala inayowakumbusha waamini Fumbo la Umwilisho na husaliwa mara tatu kwa siku: Saa 12:00 asubuhi, Saa 6:00 mchana na Saa 12:00, wakati ambapo kengele ya Sala ya Malaika wa Bwana hugongwa. Neno Malaika wa Bwana limetolewa kutoka katika Sala ya Malaika wa Bwana aliyempasha Bikira Maria kwamba, atamzaa Kristo Yesu na husaliwa Salam Maria tatu. Sala hii husaliwa na Papa kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro wakati wa Jumapili na Wakati wa Siku kuu na Sherehe. Kabla ya Sala, Papa hutangulia kutoa tafakari akifanya rejea kwa Masomo ya siku. Baadaye kunafuatia salam kwa wageni na mahujaji. Kuanzia Sherehe ya Pasaka hadi Pentekoste, badala ya Sala ya Malaika wa Bwana, waamini husali Sala ya Malkia wa Bwana, sala inayokumbuka Ufufuko wa Kristo Yesu na mwishoni, husaliwa Sala ya Atukuzwe Baba mara tatu.

Sala ya Malaika wa Bwana/ Malkia wa Mbingu ya hivi karibuni

Soma yote >