"Avvolti"ni mpango uliowakilishwa kwa Papa wa usomoji wa Sanda kupitia mfumo wa kidijiatali
Vatican News
Sanda ni kama ambavyo haijawahi kuonekana hapo awali. Tarehe 9 Januari 2026, Baba Mtakatifu Leo XIV alikuwa wa kwanza kujiunga na mpango uitwao Avvolti yaani Aliyefunikwa, ulioundwa na Jimbo Kuu la Torino nchini Italia kwa ajili ya Jubilei, ambao unatoa uzoefu wa usomaji wa kidijitali wa picha za Sanda Takatifu ya Torino, unaopatikana mtandaoni duniani kote. Programu hiyo iliwasilishwa kwa Papa na Mlinzi wa Kipapa wa Kanisa Kuu linalohifadhi Sanda Takatifu, Kardinali Roberto Repole, Askofu Mkuu wa Torino, wakati wa Mkutano iliyohudhuriwa katika Jumba la Kitume mjini Vatican.
Kuleta umma karibu na Sanda
Programu hii ni ya kwanza: itawezekana kuunganishwa na programu hiyo mtandaoni kutoka katika tovuti:www.avvolti.org kama pia Tofuti rasimi:www.sindone.org , kwa kutumoa kifaa chochote:( smartphone, tablet, pc) yaani simu mahiri ya mkono, kompyuta kibao, Kompyuta kamili, yenye ufikiaji wa kimataifa ya Kieletroniki. Shukrani kwa programu hii, unaweza "kutembelea" picha ya Sanda Takatifu kwenye skrini yako, na kuongeza maelezo muhimu zaidi (Uso, Taji la Miiba, n.k.). Kila upanuzi unaambatana na maelezo na viungo vya vifungu vya Injili vinavyoelezea Mateso ya Yesu. Usomaji wa kidijitali unakusudiwa kuleta umma kwa ujumla, duniani kote, karibu na picha ya Sanda Takatifu na maana zake. “Licha ya ukali wa kisayansi wa maandishi na picha, tumejitahidi kuunda bidhaa inayoweza kufikiwa na wote, badala ya mpango unaolenga wataalamu.”
Uzoefu wa Kidijitali wa Kimataifa
Kardinali Repole alikumbusha kwamba uchapishaji wa uzoefu wa kidijitali wa kimataifa ni sehemu ya mpango wa "Sanda ya Uchungaji" ambao Kanisa la Torino ulizindua mwaka 2024, ambao Avvolti imekuwa msingi wa Mwaka wa Jubilei 2025. Mipango mingine itapangwa na kuendelezwa katika miezi ijayo, ili kuunda safari ya kusindikiza kuelekea Jubilei ya 2033. Kipindi cha masika iliyopita ya 2025, hema la Avvolti liliwekwa kwenye Uwanja wa Castello huko Torino, kwa njia hiyo miongoni mwa vipengele vingine, hema hilo liliwasilisha usomaji wa kidijitali wa Sanda, likitoa picha hiyo kwa kipimo cha 1:1 kwenye meza yenye urefu wa mita 5 iliyoundwa maalum. Hema hilo lilitembelewa na zaidi ya watu 30,000 kutoka nchi 79 wakati wa ufunguzi wake wa siku nane (Aprili 28 hadi Mei 5).
Programu iliyowasilishwa mezani, ikiwa imebadilishwa ipasavyo, sasa inapatikana kwa kila mtu mtandaoni. Picha na maandishi kutoka kwa uzoefu yanaweza kupatikana kwenye tovuti www.avvolti.org na kwenye mitandao ya kijamii (Facebook na Instagram,).