Tafuta

2026.06.09 Papa alikutana na Familia ya Kiagostiniani huko Barcelona. 2026.06.09 Papa alikutana na Familia ya Kiagostiniani huko Barcelona.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV kwa Waagostinian wa Katalonya:wape utajiri wenu wa kiroho kwa kila mtu

Katika makazi ya Askofu Mkuu huko Barcelona,Jumanne Juni 9 Papa Leo XIV alikutana na kundi la watawa wa kike na kiume wa Shirika la Mtakatifu Agostino kutoka sehemu mbalimbali za Hispania na katika mazingira ya joto na urafiki,alitumia kama nusu saa nao.Pia walikuwepo ndugu wa Jumuiya ya Kimataifa wanaofanya huduma yao ya kichungaji katika kitongoji cha Raval cha jiji kuu la Katalonya.

Tiziana Campisi na Angella Rwezaula Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV aliwapatia mwaliko kwa takriban wanashirika 25 wa familia ya Mtakatifu Agostino aliokutana nao alasiri ya tarehe 9 Juni 2026 katika makazi ya Askofu Mkuu huko Barcelona, "Msijifungie ndani ya jumuiya zenu, bali mpeleke utajiri wa maisha yenu ya kiroho kwa kila mtu katika mazingira ya kila siku." Yamejiri akiwa  tayari katika  kituo chake cha Pili  cha hija yake ya 4 ya kitume nchini Hispania.

Papa akizungumza na Waagostiniani wa Barcelona
Papa akizungumza na Waagostiniani wa Barcelona   (@Vatican Media)

Papa Leo XIV, kulingana na chaneli ya Telegram ya Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Vatican, inabainisha kuwa, alitumia karibu nusu saa, "katika mazingira ya upendo na urafiki," pamoja na wenzake kutoka Katalonya na Wamisionari wa Kiagostinian, Watawa wa ndani wa Kiagostinian na Masisita wa Faraja wa Kiagostinian. Mwishoni mwa mazungumzo, Papa  Leo XIV alitoa baraka zake na kuwasalimu watawa hao wa kike na kiume mmoja mmoja

Waagostinian wa  Barcelona

Miongoni mwa Waagostinian waliokuwapo katika mkutano huo, ni watawa 4 wa Jumuiya ya Kimataifa wanaoishi katika Parokia ya Carme huko Barcelona,​​​​ katika Wilaya ya Raval, wanajitolea kwa huduma ya kichungaji katika Parokia za Mtakatifu Roque, Mtakatifu Agostino, Mama asiye na Dhambi na Mtakatifu Lorenzo Ruiz. Padre Dennis Pineda, Padre Michael Go Maambong, Padre Faustin John Mlelwa, Padre Laurent Joseph Temanya, hawa ni kutoka Ufilippini na Tanzania na katikati ya jiji kuu la Kikatalani, wanajitolea kwa shughuli mbalimbali. Kwa kushirikiana na kushiriki majukumu, wanatekeleza kazi yao ya kichungaji katika mazingira ya kidugu, mfano wa karama yao ya Kiagostinian.

Padre Faustin John Mlelwa,(OSA) kutoka Tanzania ni Paroko wa Parokia ya Mt.Agostino huko Barcelona
Waagostinian huko Barcelona
Waagostinian huko Barcelona   (@Vatican Media)

Shughuli za Kichungaji za Watawa

Katika Parokia ya Mtakatifu Roque, watawa, pamoja na kusimamia mipango na sherehe za uinjilishaji, wanahamasisha mipango mbalimbali ya kielimu, kijamii, na kiutamaduni inayolenga watoto, vijana, na watu wazima, hasa kwa kuzingatia makundi yaliyo hatarini. Kazi hii ya kijamii na kielimu inafanywa kwa ushirikiano na Mfuko wa  Mtakatifu Roque ambao uko katika Parokia hiyo hiyo. Pia katikati ya Barcelona, ​​​​katika Parokia ya Mtakatifu Agostino, ambapo Papa atakutana na mashirika ya upendo na usaidizi ya jimbo kuu tarehe 10 Juni 2026, watawa hawa wanawajibika kwa Katekesi na liturujia, kuongoza jumuiya za Kikristo kutoka nchi mbalimbali za Amerika Kusini ambazo husherehekea utamaduni na ibada zao hapo na kushirikiana na Mfuko wa Mano Amiga, ambao husaidia wahamiaji kwa kusambaza chakula na nguo.

Waagostinian huko Barcelona
Waagostinian huko Barcelona   (@Vatican Media)

Wahudumu wa Parokia, pamoja na kutoa mahitaji ya kiroho na kimwili ya wale wanaohudhuria Parokia, huwatunza watu wengi wa dini zingine. Hatimaye, katika Parokia ya Mama asiye na Dhambi na Mtakatifu Lorenzo Ruiz, Waagostinian wanaunga mkono Jumuiya ya Wafilipino wanaoishi katika jiji kuu la Kikatalani, wakiwapa huduma ya kichungaji waamini, wakiwasaidia katika mahitaji yao ya kiroho na kijamii. Parokia zote tatu pia zina dhamira ya kuwasindikiza wahamiaji. Waagostinian wamekuwepo Barcelona tangu karne ya 13. Konventi yao ya kwanza ilijengwa mwaka  1349 katika kitongoji cha Ribera. Leo hii, kwa kiasi kikubwa kuna kumbukumbu ya Picha ya jiji, Jumba la Makumbusho la Chokoleti, na Hoteli ya Mtakatifu Agostino. Katika karne ya 18 Waagostinian walihamia Wilaya ya Raval na hapo wanaendelea kutekeleza utume wao kwa "moyo mmoja na roho moja", wakifuata mwongozo wa Mtakatifu Agostino.


Zawadi za Watawa wa Kiagostinian

Familia ya Kiagostinian nchini Hispania imehamasishwa sana katika siku za hivi karibuni kwa ajili ya ziara ya kitume ya Papa Leo XIV. Zaidi ya watu 8,000, wakiwemo vijana, familia, na wanaume na wanawake watawa kutoka sehemu mbalimbali za nchi, walifika Madrid kati ya Jumamosi na Jumatatu ili kushiriki katika mikutano na Papa. Hata hivyo, wengi hawakuweza kusafiri hadi mji mkuu, na watawa  wa ndani wa Kiagostinian wa Seville na Huelva, lakini walitengeneza  Rozari kwa ajili yao. Ishara hii pia ilionesha mapendo yao kwa Papa Leo XIV  na kuwafanya wale waliounganishwa na jumuiya zao za watawa na wale watakaowatembelea wakati wa kukaa kwa Papa Leo XIV nchini Hispania wajisikie karibu naye.

Papa akiwabariki watawa wa kiagostino
Papa akiwabariki watawa wa kiagostino   (@Vatican Media)

Wakati wa ziara ya Papa huko Madrid, watawa wa Kiagostinan wa  Monasteri ya Mtakatifu  Isabel waliandaa biskuti zinazoitwa "pastas de San Alonso," zilizopewa jina la mwanzilishi wa Jumuiya ya watawa, Mtakatifu Alonso de Orozco. Vitumbua hivyo vilipelekwa kwa Papa,  pamoja na barua. Katika barua hiyo, watawa hao walimkumbusha Papa uwepo wao Roma  tarehe 19 Mei 2002, siku ya kutangazwa kwa Mtakatifu Alonso kuwa mtakatifu, na mkutano wao katika Uwanja wa Mtakatifu Petro pamoja naye, ambaye wakati huo alikuwa Mkuu wa Shirika la Mtakatifu Agostino.

WAAGOSTINO WA KIKATALANI

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here

09 Juni 2026, 20:00