Tafuta

2026.03.22 Kardinali Jean - Battista Pham Minh Man – Vietnam. 2026.03.22 Kardinali Jean - Battista Pham Minh Man – Vietnam. 

Papa Leo XIV amkumbuka Kardinali Pham Minh Mân:"Mhamasishaji wa umoja"

Baba Mtakatifu Leo XIV alituma salamu za rambirambi kufuatia na kifo cha Kardinali wa Vietnam kilichotokea Dominika Machi 22,akiwa na umri wa miaka 92.Papa anabainisha kuwa,"Huduma yake ya kichungaji ilioneshwa kwa dhati."Mazishi yatafanyika Ijumaa tarehe 27 Machi 2026.

Vatican News

Baba Mtakatifu Leo XIV  ameelezea "huzuni" yake kuhusu kifo cha Kardinali wa Vietnam Jean-Baptiste Pham Minh Mân, aliyekuwa Askofu Mkuu Mstaafu wa Jiji la Than-Phô Ho Chi Minh, ambaye alifariki Dominika tarehe 22  Machi 2026, juma chache baada ya kutimiza miaka 92, tarehe 5 Mahi 2026. Katika telegramu iliyotolewa tarehe 26 Machi 2026    ilikielekezwa kwa Askofu Mkuu Joseph Nguyễn Năng, wa Jiji la Ho Chi Minh, Papa alielezea rambirambi zake "kwa mapadre, watawa, na waamini walei wa jimbo kuu" na anakumbuka "kwa shukrani kubwa miaka yake mingi ya huduma ya kikuhani na kiaskofu katika makanisa ya ndani ya Jiji la My Tho na Ho Chi Minh, pamoja na michango yake kwa Kanisa huko Vietnam na kwa Vatican.

Maisha aliyoishi kwa unyenyekevu

Papa Leo XIV alisisitiza  zaidi kujitolea kwa Kardinali kwa "utunzaji wa kichungaji," ushiriki wa kijamii, na "kukuza mazungumzo na umoja wa kikanisa kila mara." Katika maandishi yake, Baba Mtakatifu aliakisi "ushuhuda wa maisha aliyoishi kwa urahisi na unyenyekevu wa kiinjili." Hatimaye, alitoa baraka zake "kama ishara ya faraja na amani katika Bwana" kwa wale wanaoomboleza kifo cha Kardinali Jean-Baptiste Pham Minh Mân, "katika tumaini la uhakika la Ufufuo."


Huduma yake ndefu ya kichungaji

Mazishi ya Kardinali yatafanyika Ijumaa tarehe 27  Machi 2026 , saa 2.30 asubuhi katika Kituo cha Kichungaji cha Jimbo Kuu la Hôchiminh Ville. Baada ya kuwa Padre akiwa na umri wa miaka 31, mnamo 1965, aliteuliwa kuwa Askofu Mwandamizi wa My Tho, mwenye haki ya urithi, na akapewa daraja la uaskofu mnamo tarehe 11 Agosti  1993. Kuanzia 2001 hadi 2007, alihudumu kama Makamu Rais wa Baraza la  Maaskofu wa Vietnam. Katika Mkutano wa  tarehe 21  Oktoba 2003, aliumbwa na kutangazwa kuwa Kardinali na Mtakatifu Yohane Paulo II, kwa kuwa na Kanisa la Roma la  Mtakatifu Justin.

RAMBI RAMBI PAPA

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku:Just click here.

 

 

26 Machi 2026, 16:40