Tafuta

Papa Leo XIV katika Groto ya Lourdes:Maria anatufudisha maana ya mateso na upendo

Mwishoni mwa Katekesi yake,kama alivyokuwa amewatangazia,Papa alikwenda kwenye Bustani za Vatican mahali palipo na Groto ya Mama Maria na kuwasha mshumaa na kusali pamoja na wagonjwa waliokuwapo katika hafla ya Siku ya Wagonjwa Duniani sanjari na sikukuu ya Mama Yetu wa Lourdes.Pia aliwaombea baraka za Mungu kwa madaktari,wauguzi na wote walio karibu na wale wanaoteseka.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Mara baada ya Katekesi yake kwenye ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican, Jumatano tarehe 11 Februari 2026, kama alivyokuwa ameeleza waamini na mahujaji, Baba Mtakatifu alikwenda katika Groto ya Lourdes iliyopo katika Bustani za Vatican katika  Siku ya Wagonjwa Duniani sanjari na Siku Kuu ya Bikira Maria wa Lourdes.


Hapo aliwakuta baadhi ya wagonjwa ambapo aliwasha mshamaa na kusali pamoja nao. Papa Leo alisema“Leo, katika siku hii iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa, tunataka kuomba kwa ushirika na wale wote wanaoteseka  ulimwenguni kote. Tunao kwa ajili yenu. Ninakushukuru kwa dhati kwa kufanya juhudi za kufika na kusindikizana nasi katika wakati huu wa maombi, hapa mbele ya mama yetu, Maria, kwenye ukumbusho wake wa kiliturujia, Mama Yetu wa Lourdes.”

Papa akiwasha Mshumaa
Papa akiwasha Mshumaa   (@Vatican Media)

“Ni siku nzuri sana inayotukumbusha ukaribu wa Maria, mama yetu, ambaye husindikizana nasi kila wakati na kutufundisha mengi: Maana ya mateso, upendo, na kusalimisha maisha ya mtu mikononi mwa Bwana.”

Papa alisali katika Groto ya Lourdes
Papa alisali katika Groto ya Lourdes   (@Vatican Media)

“Kwa hivyo, tunaomba pia baraka za Bwana kwa ajili yenu, kwa wagonjwa wote leo na siku zote, na kwa wale wote wanaowasindikiza: sayansi ya matibabu, madaktari, wauguzi, watu wengi walio karibu nasi, hasa katika nyakati ngumu zaidi. Tuombe pamoja: Salamu Maria...

Papa aliwabariki
Papa aliwabariki   (@Vatican Media)

Baraka. … Asante Mungu awasindikize daima.”

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku: Just click here.

11 Februari 2026, 16:11