Tafuta

Miaka mingi ya mgogoro wa haiti. Miaka mingi ya mgogoro wa haiti.  (AFP or licensors)

Haiti yatangaza uchaguzi mkuu wa Desemba 13,2026.

Tangazo hili linakuja baada ya miaka mingi ya mkwamo wa kitaasisi.Haiti haijafanya uchaguzi tangu 2016 na kufuatia mauaji ya Rais Jovenel Moïse mnamo Julai 2021, imeachwa bila kiongozi wa nchi aliyechaguliwa.Ratiba ya awali,ambayo ilihitaji duru ya kwanza ya upigaji kura mnamo Agosti 30 mwaka huu,ilikuwa tayari imeahirishwa. Jumuiya ya Carribiean ilikaribisha kuchapishwa kwa tarehe mpya!

Vatican News 

Mamlaka za uchaguzi za Haiti zimetangaza ratiba mpya ya uchaguzi wa rais na wabunge, wa kwanza tangu 2016. Mzunguko wa kwanza umepangwa kufanyika Desemba. Na mzunguko wa Pili unaweza kufanyika mnamo tarehe 21 Februari 2027 Hata hivyo, Baraza la Uchaguzi la Muda limefafanua kwamba kufikia tarehe hizi za mwisho kutategemea kurejeshwa kwa hali zinazokubalika za usalama na upatikanaji wa rasilimali za kifedha zinazohitajika kuandaa upigaji kura.

Hali ya kibinadamu inabaki kuwa mbaya

Usalama unabaki kuwa suala muhimu katika nchi ambapo hali ya kibinadamu ni mbaya. Kulingana na Umoja wa Mataifa, takriban watu milioni 1.5 wamehamishwa kutokana na vurugu kutoka kwa magenge yenye silaha, ambayo yanadhibiti sehemu kubwa ya mji mkuu, Port-au-Prince. Katika miezi ya kwanza ya 2026, inasemekana watu 1,600 wameuawa na mamia kujeruhiwa. Ujumbe wa Kimataifa wa usaidizi wa usalama unaoongozwa na Kenya pia unafanya kazi katika muktadha huu, lakini hadi sasa umeshindwa kunyakua udhibiti wa maeneo makubwa ya nchi kutoka katika mashirika ya uhalifu.

Uchaguzi wa kwanza tangu 2016

Tangazo hili linakuja baada ya miaka mingi ya mkwamo wa kitaasisi. Haiti haijafanya uchaguzi tangu 2016, na kufuatia mauaji ya Rais Jovenel Moïse mnamo Julai 2021, nchi imeachwa bila mkuu wa nchi aliyechaguliwa. Ratiba ya awali, ambayo iliitaka mzunguko wa kwanza mnamo Agosti 30 mwaka huu, ilikuwa tayari imeahirishwa. Jumuiya ya Carribea (CARICOM) ilikaribisha kuchapishwa kwa ratiba mpya, ikiiita hatua muhimu katika kufufua mchakato wa kidemokrasia.

OFF THE RADAR- Yale yasiyozungumzwa
28 Julai 2026, 16:30