Tafuta

2026.02.27 Brasile

Brazil:Watu kadhaa hawajulikani walipo huku Brazil ikikabiliwa na mvua kubwa

Mvua kubwa kusini mashariki mwa Brazil imesababisha vifo vya watu wasiopungua 30,huku wengine wengi zaidi wakiorodheshwa kuwa hawajulikani walipo.

Na Christopher Wells - Vatican.

Serikali ya Brazil imetambua hali ya janga huko Juiz de Fora katika jimbo la Kusini mwa Minas Gerais, ambapo mvua kubwa imewafukuza mamia ya watu. Kulingana na mamlaka mahalia, hali mbaya ya hewa imesababisha vifo vya watu wasiopungua thelathini, huku watu thelathini na tisa bado hawajulikani walipo. Dhoruba zilisababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi katika maeneo yote yaliyoathiriwa, na timu maalum za uokoaji ziko katika eneo hilo zikijibu dharura na kuwatafuta waliopotea.

“Leo letu ni kuhakikisha msaada wa binadamu”

Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva alitumia huduma ya mitandao ya kijamii X kuelezea majibu ya serikali, akiandika, "Lengo letu ni kuhakikisha msaada wa kibinadamu, urejesho wa huduma za msingi, usaidizi kwa watu wenye ulemavu, na usaidizi wa ujenzi upya." Tangazo la hali ya janga linakusudiwa kuharakisha misaada na misaada ya kibinadamu, serikali ya Brazil ilisema katika taarifa. Msimu wa mvua nchini Brazil, kuanzia Desemba hadi Machi huleta mvua kubwa kila mara, pamoja na mafuriko na maporomoko ya ardhi. Wakazi wa Juiz de Fora walisema Februari hii imekuwa na mvua kubwa zaidi katika historia ya jiji hilo. Taasisi ya Kitaifa ya Hali ya Hewa ya Brazil imetoa tahadhari za mvua kubwa Jumanne kwa sehemu za majimbo 14, ikiwa ni pamoja na Minas Gerais na Rio de Janeiro zote.

Asante kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here

 

 

02 Machi 2026, 09:37