Ukraine,Trump na Zelensky wakutana Florida
Vatican News
Matumaini ya mazungumzo hayo takuwa "yenye kujenga sana" na kwamba usaidizi wa Ulaya na Canada, uliooneshwa kwa kifurushi cha misaada cha takriban euro bilioni 1.5, utaungwa mkono na usaidizi wa Marekani. Ni kwa roho hiyo kwamba Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alijiandaa kukutana na Rais wa Marekani Trump huko Mar a Lago, Florida nchini. Mkutano huu ulifanyika miezi miwili baada ya mkutano wao wa mwisho, ambao ulifanyika mnamo Oktoba iliyopita na uligubikwa na mvutano mkubwa.
Kwa upande wa Zelensky, ambaye shambulio kubwa Desemb 27 dhidi ya Kyiv lilionesha kwamba "Putin hataki amani," itakuwa muhimu kupata makubaliano ya Trump kwa toleo jipya la mpango wa amani, ambao haushughulikii kujiondoa kwa Ukraine kutoka 20% ya eneo la mashariki la Donetsk ambalo bado liko chini ya udhibiti wake, ambalo ni hitaji kuu la Urusi la eneo. Maandishi mapya pia hayatajumuisha tena wajibu wowote wa kisheria kwa Kyiv kujizuia kujiunga na NATO, jambo lingine muhimu lililooneshwa na Kremlin.
Tishio la Lavrov
Trump na Zelenksy pia walijadili hatima ya kiwanda cha nyuklia cha Zaporizhia kinachodhibitiwa na Urusi, pamoja na dhamana za usalama ambazo Magharibi zinaweza kutoa kama sehemu ya makubaliano ya amani yanayowezekana. Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen alisisitiza Jumamosi Desemba 27 kwamba makubaliano hayo lazima yahifadhi "uhuru" na "uadilifu wa eneo" la Ukraine. Wakati huo huo, Moscow ilishutumu Kyiv na Ulaya kwa kujaribu "kupigia upatu mpango wa awali uliosimamiwa na Marekani wa kukomesha mapigano.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Lavrov alitangaza kwamba "ikiwa mtu yeyote ataamua kushambulia Urusi, majibu yatakuwa mengi." Warusi, wakati huo huo, wametangaza kwamba wameteka miji mingine miwili mashariki mwa Ukraine. Baada ya shambulio kubwa dhidi ya Kyiv kwa kutumia ndege zisizo na rubani na makombora kadhaa, ambayo yalisababisha vifo vya watu wawili, umeme umeripotiwa kurejeshwa kwa nyumba zote katika mji mkuu wa Ukraine. Mashambulizi yalitokea Desemba 27, usiku huko Kherson, yakilenga maeneo ya makazi na miundombinu muhimu, na kuacha sehemu ya jiji bila umeme.
Wakati huo huo, matengenezo makubwa ya njia za umeme yameanza karibu na mtambo wa nyuklia wa Zaporizhia, kufuatia makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoratibiwa na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki. Matengenezo haya yanatarajiwa kudumu kwa siku kadhaa na yanafuatiliwa na timu ya IAEA.