Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Kijé's death
Ratiba Podcast
Israel yasitisha kutoa msaada huko Gaza. Israel yasitisha kutoa msaada huko Gaza.  (AFP or licensors)

Israel yasitisha Msaada kwa Gaza hadi Hamas ikubali mpango

Marekani inaunga mkono uamuzi wa Israel wa kusitisha misaada ya moja kwa moja ya kibinadamu kwa Ukanda wa Gaza na kufunga vivuko vya mpaka hadi Hamas iwaachilie mateka.Mwitikio wa Umoja wa Mataifa unabainisha kuwa ni:“uamuzi wa kutisha.”

Na Angela Rwezaula – Vatican.

Ni Uamuzi, wa Israeli wa kusimamisha uingiaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza  ambapo Israel itajiondoa ikiwa Hamas haitakubali kile kinachoitwa "mpango wa Witkoff", ulioandaliwa na mjumbe wa Marekani katika Mashariki ya Kati, ambao unatoa muda wa kurefushwa kwa awamu ya kwanza ya makubaliano ya mapatano katika Gaza ya takriban siku 50, ikijumuisha kipindi chote cha Ramadhani - mwezi mtukufu kwa Kiislamu ulioanza Machi 1 - na Pasaka ya Kiyahudi. Wakati wa awamu hii, kundi la Kiislamu linatarajiwa kuwaachilia mateka ambao bado wako hai, karibu 24 na kukabidhi miili ya marehemu.

Nafasi za kimataifa

Lawama hizo zilikuwa kali kutoka katika nchi za Kiarabu, ikiwa ni pamoja na Misri - mmoja wa wapatanishi wakuu wa usitishaji mapigano - na pia kutoka Umoja wa Mataifa, ambao kupitia msemaji wake Tom Fletcher aliuita uamuzi wa Israeli "wa kutisha," ukizingatia kwamba sheria ya kimataifa ya kibinadamu inaweka wazi kwamba ufikiaji wa misaada lazima uruhusiwe. Kusitishwa kwa msaada huo, kunaungwa mkono na urais wa Marekani wa Trump, ambaye, kupitia kwa msemaji wa Baraza la Usalama la Taifa Ikulu (White House,) Brian Hughes, alisema kuwa "Israel imejadiliana kwa nia njema tangu mwanzo wa utawala huu ili kupata kuachiliwa kwa mateka". Katika shutuma za Hamas kwamba Israel inawasababishia njaa wakazi wa Gaza, Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Sa'ar alisema kwamba wakati wa mapatano ya majuma sita, vifaa vya kutosha kwa takriban miezi minne viliingia Ukanda huo.

03 Machi 2025, 13:24
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031