Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Cuban Ouverture
Ratiba Podcast
Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa pamoja wa EAC-SADC kuhusu mgogoro wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa pamoja wa EAC-SADC kuhusu mgogoro wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.  (ANSA)

Tanzania:Maamuzi ya EAC na SADC katika mkutano kuhusu mzozo DRC!

Njia ya kupeleka misaada ya kibinadamu lazima ifunguliwe haraka,Serikali ya DRC irejee katika meza ya mazungumzo na makundi ya waasi,Jumuiya ya Kimataifa iunge mkono juhudi za kuleta amani,Mkutano wa EAC na SADC uwe na vikao vya aina hiyo angalau mara moja kwa mwaka ili kujadili maendeleo ya utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa.Haya na mengine yaliibuka katika maazimio ya Mkutano wa SADC na EAC uliozungumzia mzozo wa mashariki mwa DRC Februari 8,Tanzania.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) walifanya maamuzi yatakayosaidia kurejesha amani  katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), iliyogubikwa na mzozo wa muda mrefu sana. Mkutano huo wa pamoja uliofanyika jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania, kwa kukaribishwa sana na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, Jumamosi tarehe 8 Februari 2025  na ambao ulihudhuriwa na wakuu wa nchi na serikali kutoka mataifa wanachama wa EAC na SADC,  ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa EAC, Rais William Ruto, wa Jamhuri ya Kenya na Mwenyekiti wa SADC, Rais Emmerson Mnangagwa wa Jamhuri ya Zimbabwe,  japokuwa hapakuwapo Rais wa Congo DRC, Bwana  Felix Tshisekedi ambaye alishiriki kwa njia ya Mtandao.

Mwenyekiti wa EAC Rais Ruto wa Kenya
Mwenyekiti wa EAC Rais Ruto wa Kenya   (ANSA)

Njia ya misaada ya kibinaadamu kazima ifunguliwe haraka

Baada ya majadiliano ya kina,  Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), walikubaliana kuwa mgogoro wa mashariki mwa DRC unaweza kutatuliwa kwa njia ya kisiasa, kidiplomasia,na hatua za kiusalama. Akisoma maazimio ya Mkutano huo Katibu Mkuu wa EAC, Bi Veronica Nduva alisema kuwa mkutano umeamua kuwa pande zote zinazozozana katika mgogoro huo zisitishe mapigano mara moja na kuweka silaha chini bila masharti yoyote. Viongozi walisisitiza kuwa njia za misaada ya kibinadamu lazima zifunguliwe haraka ili kuruhusu upatikanaji wa chakula, dawa, na huduma nyingine muhimu kwa wananchi walioathiriwa na mapigano. Ili kuhakikisha hali ya usalama inarejea, wakuu wa majeshi wa EAC na SADC wamepewa siku tano kuandaa mpango wa Ulinzi wa Goma na maeneo yanayozunguka jiji hilo. Hatua hii inalenga kuzuia mashambulizi zaidi na kuwalinda wananchi walio katika hatari ya kushambuliwa na waasi.

Serikali ya DRC irejee katika meza ya mazungumzo na makundi ya waasi

Hata hivyo kwa upande wa Katibu Mkuu huyo alisema kwamba kwa  upande wa mazungumzo ya amani, viongozi wa EAC na SADC waliamua kuwa serikali ya DRC irejee kwenye meza ya mazungumzo na makundi yote, yakiwemo ya kijeshi na yasiyo ya kijeshi, chini ya mwavuli wa mchakato wa Nairobi na Luanda. Kwa hiyo walikubaliana pia kuwa juhudi zote za amani zinazofanyika ziunganishwe kuwa mpango mmoja ili kuharakisha upatikanaji wa suluhisho  la kudumu. Viongozi wa mkutano huo wameagiza kuondolewa kwa vikosi vyote vya kigeni visivyoalikwa kutoka ardhi ya DRC. Ili kuhakikisha utekelezaji wa hatua hiyo, wameagiza kufanyika kwa kikao cha pamoja cha Mawaziri wa Ulinzi wa EAC na SADC ndani ya siku 30 zijazo ili kuweka mkakati madhubuti wa utekelezaji.

Jumuiya ya Kimataifa iunge mkono  juhudi za kuleta amani

Katika maamuzi pamoja na hayo, viongozi hao walisisitiza kuwa suluhisho la kudumu kwa ajili ya mgogoro huo wa DRC lazima lijikite katika ushirikiano wa kisiasa na kidiplomasia. Kwa hiyo walisisitizia “Jumuiya ya kimataifa kuwa inapaswa kuunga mkono juhudi zakuleta amani, hasa kwa kusaidia juhudi za kidiplomasia na kuzuia uungwaji mkono wa makundi ya waasi.” Hatimaye Mkutano huo wa Vingozi wa EAC na SADC pia uliazimia “kuwa vikao vya aina hiyo viwe vinafanyika angalau mara moja kwa mwaka ili kujadili maendeleo ya utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa na kuhakikisha kuwa mchakato wa kurejesha amani nchini Jamhuri ya Congo (DRC )unaendelea kwa kasi inayotakiwa.”

09 Februari 2025, 10:28
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031