Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Rondeau (Allegro)
Ratiba Podcast
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rubio akiwa mezani na Waziri wa Urusi Lavrov huko Riyadh. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rubio akiwa mezani na Waziri wa Urusi Lavrov huko Riyadh.  

Mazungumzo ya Marekani na Urusi yaanza mjini Riyadh.Kiev haitambui meza

Mazungumzo kati ya wajumbe wa Marekani na Urusi kuhusu uwezekano wa kumaliza vita nchini Ukraine yameanza nchini Saudi Arabia tarehe 18 Februari 2025.Mkutano huo unafanyika katika moja ya jumba la Albasatin la familia ya kifalme ya Saudi Arabia.

Vatican News

Wajumbe wa Marekani na Urusi wamekuwa katika mji mkuu wa Saudia Arabia tangu Jumatatu jioni tarehe 17 Februari 2025 ambapo wanafanya Mkutano Jumanne tarehe 18 Februari. Waziri Lavrov anaongoza ujumbe wa Moscow, ambao pia unajumuisha Yuri Ushakov na oligarch Kirill Dmitriev washauri wa kidiplomasia wa Kremlin(Urusi). Wawakilishi wa utawala wa Marekani ni Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio, Mshauri wa Usalama wa Taifa Mike Waltz na Mjumbe wa Mashariki ya Kati Steve Witkoff.

Lavrov: Hapana kuwa na makubaliano ya eneo kwa Ukraine

Maneno yaliyotolewa na Rubio usiku wa kuamkia Jumanne 18 Februari 2025 yanaonekana kutaka kuwahakikishia washirika wa Ulaya na Kyiv: "Mkutano sio meza ya mazungumzo ya kuamua amani ya Ukraine, lakini ni mwanzo tu wa kutoa ubaridi  kati ya nchi hizo mbili, anasisitiza Katibu wa Nchi kuwa,  Ulaya hakika itahusika katika mazungumzo." Maneno ya Lavrov yalikuwa ya asili tofauti kabla ya kuwasili Riyadh, alisema kwamba hakuna makubaliano ya eneo yangefanywa kwa Ukraine na kwamba hakukuwa na nafasi mezani kwa "wa Ulaya wanaotaka kurefusha vita." Wakati huo huo Rais wa Ukraine Zelensky kwa upande wake alimsuta Trump akisema anataka kumfurahisha Putin. "Kwa sasa, meza hii haipo kwa ajili yetu," aliongeza Mychailo Podolyak, mshauri wa kwanza wa rais wa Ukraine.

Ulaya iligawanyika

Viongozi wa Ulaya waliokutana mjini Paris tarehe 17 Februari 2025, walisalia kuwa  na mgawanyiko kuhusu iwapo watatuma wanajeshi wa kulinda amani nchini Ukraine. Ufaransa, Italia, Ujerumani, Hispania, Uingereza, Denmark, Poland na Uholanzi zilijikuta  kwenye safu tu ya jumla ya msaada kwa Kiev. Baada ya mkutano huo katika mji mkuu wa Ufaransa, Rais Macron alifanya mazungumzo ya simu na Trump na Zelensky, ambapo mwisho wake aliandika ujumbe katika X kwamba amani ya kudumu lazima Urusi ikomeshe uchokozi wake na hii lazima iambatane na dhamana kali na za kuaminika za usalama kwa Waukraine: “Tutashughulikia hili na wa Ulaya  wote, Wamarekani na Waukraine."

18 Februari 2025, 12:32
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031