Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Rondeau. Tempo di Menuetto
Ratiba Podcast
Hawa ni watoto wa kambi ya wakimbizi ya ndani huko Mitwaba,Congo DRC. Hawa ni watoto wa kambi ya wakimbizi ya ndani huko Mitwaba,Congo DRC. 

Maghala ya chakula Mashariki mwa DRC ya WFP yameporwa

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani (WFP)tarehe 17 Februari 2025 limelaani vikali uporaji wa chakula huko DRC na kuonya kuwa uporaji huu utazidisha hali mbaya ya kibinadamu katika eneo hilo la Mashariki ambako hali inazidi kuwa tete. Licha ya changamoto hii, WFP imesisitiza kuwa iko tayari kuanza tena ugawaji wa msaada wa chakula mara tu hali ya usalama itakapokuwa imerejea.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani (WFP) tarehe 17 Februari 2025 limelaani vikali uporaji wa maghala yake ya chakula mjini Bukavu, Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC.) Katika taarifa yake fupi ilyotolewa mjini Geneva shirika hilo limesema “Chakula kilichoibwa kilikuwa kimekusudiwa kusaidia familia zilizo hatarini zaidi wakati ghasia zinaendelea kuenea na upatikanaji wa chakula ukiwa mgumu zaidi.”

Uporaji utasababisha hali mbaya ya kibinadamu

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani limeonya kuwa uporaji huu utazidisha hali mbaya ya kibinadamu katika eneo hilo la Mashariki ambako hali inazidi kuwa tete. Licha ya changamoto hii, WFP imesisitiza kuwa iko tayari kuanza tena ugawaji wa msaada wa chakula mara tu hali ya usalama itakapokuwa imerejea. Shirika hilo limehimiza hitaji la dharura la kurejesha utulivu katika maeneo yaliyoathirika ili wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu waweze kuwafikia wahitaji kwa usalama. Hata hivyo, ghasia zinazoendelea limesema shirika hilo zinaendelea kuwa kikwazo kikubwa kwa juhudi za usambazaji wa misaada ya kibinadamu. WFP imetoa wito kwa pande zote zinazohusika katika mgogoro unaoendelea DRC kuheshimu sheria za kimataifa za kibinadamu. “Hii inajumuisha ulinzi wa raia, wahudumu wa misaada ya kibinadamu, na mali za kibinadamu ili kuhakikisha msaada wa kuokoa maisha unawafikia wanaouhitaji.”

Mashambulizi dhidi ya misaada ya kibinadamu ni moja ya hatari kwa mamilioni ya watu 

Shirika hilo pia limeeleza kuwa mashambulizi dhidi ya misaada ya kibinadamu yanahatarisha moja kwa moja maisha ya mamilioni wanaotegemea msaada huo ili kuendelea kuishi. Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani(WFP),tukio hili la uporaji linajiri wakati ambapo mgogoro wa chakula unazidi kuwa mbaya katika eneo la mashariki mwa DRC, ambako ghasia zinazoendelea zimewalazimu maelfu ya watu kuyahama makazi yao na kuathiri vibaya minyororo ya usambazaji wa chakula. Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani(WFP) inatoa wito wa msaada wa haraka kutoka kwa Jumuiya ya Kimataifa ili kurejesha operesheni za kibinadamu na kuzuia mateso zaidi katika moja ya maeneo yaliyo hatarini zaidi kwa ukosefu wa chakula duniani.

17 Februari 2025, 17:38
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031