Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Allegro
Ratiba Podcast
Watu wa Palestina wakiwa njiani kurudi nyumbani kwaho Kaskazini mwa Gaza. Watu wa Palestina wakiwa njiani kurudi nyumbani kwaho Kaskazini mwa Gaza. 

Israel yajiondoa kwenye Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa

Waziri Saar anashutumu Umoja wa Mataifa kwa ubaguzi na propaganda za chuki dhidi ya Wayahudi.Wakati huo huo,kuna kilio cha kimataifa kuhusu wazo lililotolewa na rais wa Marekani la kuwahamisha Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza ili kuugeuza kuwa "Pwani ya Mashariki ya Kati".

Na Angella Rwezaula - vatican 

Israel itafuata mfano wa Marekani na kujiondoa katika Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa. Uamuzi huo uliotangazwa kupitia mitandao ya kijamii na Waziri wa Mambo ya Nje Gideon Saar haukukosi utata: "Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa kiutamaduni limewalinda wanaokiuka haki za binadamu huku likitilia shaka demokrasia pekee ya Mashariki ya Kati: Israel," alisema Saar.

Ufafanuzi kuhusu mpango wa Trump kwa Gaza


Wakati huo huo, upinzani wa kimataifa unazidi kukua kwa mpango wa Rais Trump kwa mustakabali wa Ukanda wa Gaza. Ndani ya masaa 24 baada ya tangazo hilo, mkuu wa Ikulu ya Marekani alitoa ufafanuzi: kwanza kabisa, kwamba hakuwa na ahadi yoyote ya kutuma wanajeshi wa Kiamerika huko Gaza na akataja kwamba uhamisho wa Wapalestina kwenda nchi zingine utakuwa wa muda mfupi ili kutekeleza urejeshaji wa eneo hilo.

 Ulimwenguni wachachamaa na tamko la Trump


Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran naye pia alilaani pendekezo la Mkuu wa Ikulu ya White House, na kulitaja pendekezo la kuwaondoa kwa nguvu Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza "ni la kushtua." Kwa upande wa Jordan na Misri, nchini ambazo ni tajiri alizitaja kuwa ndizo zinazofaa zaidi kuwakaribisha Wapalestina katika Ukanda huo, tayari zilikuwa zimekataa kwa nguvu dhana yoyote katika mwelekeo huu. Urusi, China na Ulaya pia hazikukubaliana, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Antonio Guterres akikumbuka kwamba "harakati zozote za kulazimishwa za watu ni sawa na mauaji ya kikabila". Maoni yote ambayo ni pamoja na yale ya pande zinazohusika: rais wa Mamlaka ya Kitaifa ya Palestina, Mahmoud Abbas, alikuwa amepinga kukataa kwa wazi, akisisitiza kwamba "haki halali za Wapalestina haziwezi kujadiliwa" wakati Hamas ilizungumza hata "msimamo wa kibaguzi".

 

06 Februari 2025, 10:17
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031