Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Cadiz
Ratiba Podcast
Watu wakikimbia nchi yao inayoendelea na ghasia kati ya Jeshi la Congo na waasi wa M23. Watu wakikimbia nchi yao inayoendelea na ghasia kati ya Jeshi la Congo na waasi wa M23. 

Congo DRC:M23 yabeba tani 10 za madini ya kimkakati kutoka eneo la Kivu Kusini

Kulingana na taarifa usiku kati ya 19 na 20 Februari 2025,kiwanda cha kuchakata madini cha kampuni za CJX kiliporwa na watu wenye silaha wa M23. Wanamgambo hao walizima kamera za uchunguzi na kuteka nyara na kutoweka maafisa wa usalama katika kituo hicho.Kwa hiyo shehena ya takriban tani 10 za madini ya aina tatu ambayo tayari yalikuwa yameandikwa na kuuzwa nje ya nchi yaliwekwa mikononi mwao:wolframite,tungsten na coltan.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Zaidi ya tani 10 za madini ya kimkakati zilinaswa na wanamgambo wa M23 kutoka kituo cha Kivu Kusini. Haya yamesemwa katika barua iliyotumwa kwa Shirika la Habari za Kimisionari Fides na "Kikundi Kazi cha Mada kuhusu Migodi na Hidrokaboni za Mashirika ya Kiraia huko Kivu Kusini." Mkoa huu ulioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) pamoja na Kivu Kaskazini, hatua kwa hatua unashindwa na wanamgambo wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.

Kupora kampuni ya madini ya CJX

Kulingana na dokezo hi "usiku kati ya tarehe 19 na 20 Februari 2025, kiwanda cha kuchakata madini cha kampuni ya CJX kiliporwa na watu wenye silaha wa M23". Wanamgambo hao walizima kamera za uchunguzi na "kuteka nyara na kutoweka maafisa wa usalama" katika kituo hicho. Kulingana na taarifa zilizokusanywa na kikundi cha mashirika ya kiraia ya Congo, "wanamgambo walikamata shehena ya takriban tani 10 za madini ya 3T ambayo tayari yalikuwa yameandikwa na tayari kuuzwa nje ya nchi.

Madini ya Kimkakati yanayosafirishwa kutoka Congo kwenda nchi za Nje

Madini ya (3T) Cassiterite (bati) wolframite(tungsten ),coltan (tantalum), ni madini matatu ya kimkakati kwa tasnia ya kielektroniki, anga na kijeshi ulimwenguni kote, ambayo ndiyo kitovu cha vita mashariki mwa DRC. Na CJX Minerals ni kampuni ya Madini ya kibinafsi chini ya sheria ya Congo, iliyoundwa mwaka wa 2014 na ndiyo msafirishaji mkuu wa madini haya (3T), katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

27 Februari 2025, 15:09
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031