Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Rondo (Allegro)
Ratiba Podcast
Wakimbizi kutoka kivu kuelekea Burundi. Wakimbizi kutoka kivu kuelekea Burundi.  (AFP or licensors)

Baada ya M23 kuingia Bukavu,mamia elfu ya watu wanakimbilia Burundi

Machafuko katika mji mkuu wa Kivu Kusini baada ya kuingia kwa waasi wa kundi la M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.Zaidi ya watu 10,000 waliokimbia makazi yao walikimbilia kuvuka Mto Ruzisi kuelekea Burundi.Wakati huo huo,mjini Kinshasa,Rais Felix Tshisekedi ameitisha mkutano kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Wakati mapigano yalipozidi kushika kasi katika Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC), biashara mjini Bukavu bado zimefungwa, huku baada ya waasi wa M23 kuingia mjini, baadhi ya watu bado wanaonekana wakitembea barabarani, wakiwa wamegubikwa na ukimya wa viziwi. Hali katika mji mkuu wa Kivu Kusini inaelezewa na chanzo kutoka shirika la Habari za Kimisionari la Fides kulingana na ambao ufyatulianaji risasi ulikoma baada ya waasi wanaoungwa mkono na Rwanda kuingia jijini Ijumaa tarehe 14 Februari 2025 mchana. Kuanguka kwa Bukavu kunafuatia mji ule wa Goma, mji mkuu wa Kivu Kaskazini, unaokaliwa sasa na M23 tangu mwishoni mwa mwezi Januari, wakati ilichukuliwa Kavumba na uwanja wake wa ndege.

Wakimbizi nchini Burundi

Kusonga mbele kwa waasi huko Kivu Kusini tayari kumesababisha maelfu ya watu waliokimbia makazi yao, wakati Vikosi vya Wanajeshi vya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimetelekeza Bukavu kwa haraka. Sehemu ya jiji iliachwa bila umeme, wakati shirika la Fides likiripoti uporaji hasa huko Kadutu, wilaya ya kihistoria ambayo soko kuu la ndani linapatikana. Wakimbizi hao walikimbia kutoka eneo la Kamanyola, kuvuka Mto Ruzisi, na kuweka kambi katika jimbo la kaskazini-magharibi la Burundi la Cibitoke. Waziri wa Mambo ya Ndani wa Congo Martin Niteretse pia alithibitisha kwamba wakimbizi wengi wameingia Burundi, lakini serikali bado haijatoa idadi zinazohusiana na mtiririko huu wa wakimbizi. Waziri huyo aliongeza hivi: “Wakongo wengi walikimbia kwa sababu waliogopa walipojua kwamba jiji la Bukavu lilikuwa limetekwa.”

Mgogoro wa kibinadamu ambao unatia wasiwasi

Kwa tahadhari, kivuko muhimu cha mpaka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Burundi kilifungwa kwa muda mfupi tarehe 16 Februari ili kuzuia wimbi kubwa la wakimbizi. Kinshasa na Gitega zimekuwa na ushirikiano mzuri baina ya nchi hizo kwa miaka mingi, na tangu mwaka 2023, jeshi la Burundi limetuma takriban wanajeshi 10,000 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kusaidia mapambano dhidi ya zaidi ya makundi 100 yenye silaha ambayo yamekithiri katika eneo hilo. Wakati huo huo, mjini Kinshasa, Rais Felix Tshisekedi ameitisha mkutano wa usalama kujadili mabadiliko ya operesheni za kijeshi katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini, pamoja na hali mbaya ya kibinadamu inayoendelea mashariki mwa nchi hiyo.
 

18 Februari 2025, 09:48
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031