Ask.Mkuu Gallagher,Nigeria,Misa ya miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia!
Vatican News
Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, anahitimisha safari yake kwenda nchini Nigeria, Jumanne tarehe 7 Julai 2026. Askofu Mkuu aliondoka kuelekea nchi hiyo barani Afrika mnamo tarehe 2 Julai, kwa ajili ya sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Vatican na Jamhuri ya Shirikisho La Nigeria, eneo ambalo lina Wakatoliki zaidi ya milioni 30 na mapadre Katoliki zaidi ya 10,000, na linakabiliwa na changamoto nyingi kwa usalama wa ndani wa watu.
Wakati wa ziara yake, kama ilivyoripotiwa na akaunti rasmi ya Sekretarieti ya Vatican X, @TerzaLoggia, Askofu Mkuu Gallagher alikutana na Rais Bola Ahmed Tinubu katika Jumba la Rais. Pia walikuwepo Bianca Odumegwu Ojukwu, Waziri wa Mambo ya Nje, na Omar Louray, Rais wa Tume ya ECOWAS(Umoja wa Kiuchumi na Kisiasa wa Nchi za Afrika Magharibi).
Baada ya kuzungumza na mwakilishi wa Vatican, Tinubu aliviambia vyombo vya ndani vya habari kwamba, alisisitiza kujitolea kwa serikali katika kuweka kipaumbele cha mazungumzo kati ya dini na kuhamasisha amani, maelewano na uvumilivu miongoni mwa jamii tofauti za kidini.
Ratiba ya usafiri ya Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa pia ilijumuisha maadhimishoya Misa Dominika tarehe 5 Juni 2026, katika Kanisa Kuu la Mama Yetu, Malkia wa Nigeria huko Garki (Abuja), kwa ajili ya shukrani ya miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.