Maadhimisho ya Miaka 100 ya Papa Benedikto XVI:Mipango ya kumkumbuka Joseph Ratzinger
Vatican News
Unaandaliwa mpango mpana wa Kimataifa wa mipango unaendelea kusherehekea miaka mia moja ya kuzaliwa kwa Papa Benedikto XVI, ambayo itakuwa mnamo tarehe 16 Aprili 2027. Matukio zaidi ya kumi yamepangwa katika mwaka mzima wa 2026, yameenea katika mabara manne, kwa lengo la kukumbuka na kuchunguza sura na mawazo ya Joseph Ratzinger. Mipango hiyo, iliyozinduliwa na Mfuko wa Vatican uliopewa jina lake, unaoratibiwa na Kamati ya Kimataifa ya Sherehe za Miaka Mia Moja iliyoanzishwa ndani ya Mfuko wenyewe.
Sehemu za kufanyika matukio
Matukio yamepangwa kufanyika Austria, Ufaransa, Italia, Uhispania, Hungaria, India, Colombia, Marekani, na Kenya. "Mwaka wa mia moja wa kuzaliwa kwa Ratzinger," alisema Padre Roberto Regoli, Rais wa Mfuko wa Ratzinger na Kamati ya Miaka Mia moja, "ni fursa ya kuwasilisha kikamilifu mawazo yake na mbinu yake ya uhalisia, kama michango muhimu kwa mjadala wa sasa wa kikanisa na kitamaduni. Urithi wake unahusu tafsiri ya Mtaguso wa Pili wa Vatikan, uzoefu binafsi wa Kristo, ambao unakuwa ufunguo wa matawi yote ya Taali Mungu, na ya busara kama kigezo kinachoongoza tafakari ya kibinadamu kuhusu uhalisia."
Ufunguzi wa miaka 100 jijini Roma
Mnamo tarehe 16 Aprili 2026, siku ya ufunguzi wa miaka mia moja, uwasilishaji wa vitabu vya Maandiko ya Joseph Ratzinger-Benedict XVI, vyenye kichwa: "Imani ya Wakati Ujao. Wakati Ujao wa Kanisa," kwa kuchapishwa na nyumba ya Vitabu ya Cantagalli, ilifanyika katika Ubalozi wa Vatican Roma. Matukio ya 2026 yatahitimishwa na Kongamano la Kimataifa la kila mwaka la Mfuko huo, lililopangwa kufanyika mnamo Novemba tarehe 18-21 katika Chuo Kikuu cha Tangaza jijini Nairobi, Kenya, kwa mada: "Constellections of Hope: Africa and the Renewal of the Church in the Vision of Benedict XVI.," yaaani "Mkusanyiko wa Matumaini: Afrika na Upyaisho wa Kanisa katika Maono ya Benedikto XVI." Kongamano hilo litafanyika kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Maria huko Minnesota, kuadhimisha miaka 40 ya Chuo Kikuu cha Tangaza. Hatimaye, sherehe ya Tuzo ya Ratzinger itafanyika Desemba 2026. Tarehe za matukio ya 2027 zitatangazwa baadaye.
Programu ya mipango mwaka wa 2026 (kwa mpangilio wa matukio)
Italia
Roma, Aprili 16, Ubalozi wa Italia wa Vatican. Katika hafla ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Miaka Mia Moja, uwasilishaji wa vitabu vinne: "Maandishi Yaliyochaguliwa" na Joseph Ratzinger-Benedikto XVI,Kichwa: Imani ya Wakati Ujao/ mstakabali. Wakati Ujao/ mstakabali wa Kanisa (Cantagalli, 2026).
Austria
Heiligenkreuz (Vienna), Machi 11-Mei 20, Chuo Kikuu cha Falsafa na Taali Mungu cha Benedict XVI: mfululizo wa mihadhara na Padre Hermann Geißler FSO, yenye kichwa cha habari "Kardinali Joseph Ratzinger kama Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa ya Mafundisho ya Imani."
Italia
Gemonio (Como), Juni 23, Kanisa la Mtakatifu Pietro (karne ya 7): Mkutano "Joseph Ratzinger-Benedikto XVI: Urithi na Umuhimu Miaka Mia Moja Baada ya Kuzaliwa Kwake," kwa ushirikiano na Jimbo la Como na Manispaa ya Gemonio.
India
Bangalore, Julai 10-11, Baraza la Maaskofu Katoliki la India, Maaskofu-Wataalimungu, Kongamano kuhusu mada: "Kusomwa upya kwa Safari ya Kitaalimungu ya Joseph Ratzinger".
Hungaria
Budapest, Septemba 10, Chuo Kikuu Katoliki cha Péter Pàzmàny: Siku ya Mafunzo wakati wa uwasilishaji wa Toleo la tatu la Kazi Kamili ya Joseph Ratzinger kwa Kihungaria: Mungu wa Imani na Mungu wa Wanafalsafa. Sababu ya Kifalsafa - Utamaduni - Ulaya - Jamii.
Colombia
Bogotá, Septemba 24-26, Chuo Kikuu cha Sabana, Kituo cha Utafiti cha Ratzinger: Mkutano wa Kimataifa "Kwa Maadhimisho ya Miaka Mia Moja ya Joseph Ratzinger: Njia za Imani, Tumaini, na Huruma."
Ufaransa
Paris, Oktoba 14, Chuo cha Bernardins, Chuo Katoliki cha Ufaransa, Taasisi ya Ufaransa, Revue "Communio," KTO: Kongamano la Kimataifa "Mihadhara Mikuu ya Joseph Ratzinger-Benedikto XVI nchini Ufaransa" (jina la muda).
Austria
Vienna, Oktoba 22-24, Chuo Kikuu cha Vienna na Chuo Kikuu cha Augsburg: Kongamano la Kimataifa "Taalimungu ya Joseph Ratzinger huko Widerstreit. Uwazi - Uandishi - Mila: Kanuni za Msingi za Taali Mungu ya Katoliki."
Hispania
Almeria, Oktoba 28-30, Kongamano la Kimataifa "Uzuri wa Liturujia" na kuzinduliwa kwa sanamu kwa ajili ya Benedikto XVI.
Marekani
Minneapolis, Novemba 3, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Maria cha Minnesota: Uwasilishaji wa Kitabu ccha Kazi zilizokusanywa za Joseph Ratzinger: Yesu wa Nazareti, kwa ushirikiano na "Word on Fire Academic" na Mwenyekiti wa Chuo Kikuu cha Benedikto XVI.
Jimbo la Winona-Rochester, Novemba 4-6, Mkutano wa Mwaka wa Rasilimali Mpya kuhusu mada: "Joseph Ratzinger na Vyanzo Vyake," kwa ushirikiano na Word on Fire Academic na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Maria.
Kenya
Nairobi, Kenya, Novemba 18-21, Chuo Kikuu cha Tangaza: Kongamano la Kimataifa la Mwaka la Mfuko huo, kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Tangaza na Chuo Kikuu cha Mtakatifu Maria cha Minnesota kuhusu mada: "Constellations of Hope: Afrika na Upya wa Kanisa katika Maono ya Benedict XVI."
Mji wa Vatican
Desemba (tarehe itaamuliwa): Sherehe ya Tuzo ya Ratzinger ya 2026.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.