Gari la Papa nchini Marekani:safari ya mshikamano kwa watoto wahanga wa vita
Na Benedetta Capelli – Vatican.
"Upendo, msingi wa maisha ya Kikristo, haupaswi kubaki kuwa suala la nadharia, bali lazima litekelezwe kwa vitendo, liwe huduma." Maneno ya Askofu Mkuu Luis Marín de San Martín, yalielezea wazi maana ya mpango huu mpya wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo, ambalo limekuwa likifanya kazi chini ya agizo la Papa. Tarehe 28 Aprili 2026, Mkuu wa baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo alimkabidhi funguo za Popemobile Michele Sagarino, rais wa shirika la upendo la Marekani "Cross Catholic Outreach," ambapo asubuhi tarehe 29 Aprili rais aliweza kumsalimia Papa Leo XIV mwishoni mwa Katekesi yake, akielezea jukumu la shirika hilo, ambalo pia limesaidia Jimbo la Chiclayo hapo awali.
Hatua hiyo iliashiria mwanzo wa: "American Catholic Heroes: "Mashujaa Wakatoliki wa Marekani:Safari ya Barabarani ya Matumaini," yapata kilomitia 3,700 kutoka New York hadi California, ili kuwasaidia watoto na watu walio katika mazingira magumu wanaopitia matokeo ya vita moja kwa moja, lakini pia kuunda fursa za maombi. Shirika hilo hilo litaandaa, kuhamasisha, na kusimamia mnada mkubwa wa upendo nchini Marekani, huku mapato yakienda kwa kazi za upendo za Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo.
Mshikamano na Uinjilishaji
Kulingana na Askofu Mkuu Luis Marín de San Martín, mpango wa kutoa Gari la Papa una thamani ya kijamii katika suala la mshikamano na wale wanaohitaji zaidi na pia unatumika "kuimarisha uhusiano na Baba Mtakatifu na kuhamasishaji." "Ninashukuru kwa Ufikiaji wa Wakatoliki Wote," alisema "ambao umeshirikiana kwa muda mrefu na Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo kwa kuunga mkono kwa ukarimu." Kazi ya shirika hilo la upendo, lililoanzishwa karibu miaka 25 iliyopita, inaenea hadi sehemu mbalimbali za dunia, ikiingilia kati katika nchi 32 mwaka 2024 pekee, ikiwa ni pamoja na Malawi, Zambia, na Haiti, likiunga mkono miradi 279, kuwekeza katika programu za afya na kilimo, kutoa chakula, maji, elimu, na, zaidi ya yote, msaada wa kiroho.
“Gari la Matumaini”
Gari la Papa kwa waandaaji wa mpango uliotangazwa, kwa hivyo, litakuwa barabarani nchini Marekani, ‘gari la matumaini,’ kwa sababu inawafikia wale wanaoteseka. Mpango huo, ambao utafanyika kati ya Juni na Julai 2026, unaendana na maadhimisho muhimu ya miaka 250 ya kusainiwa kwa Azimio la Uhuru la Marekani mwaka 1776. Litatembelea miji 13 ikiwemo New York na Washington, ukisimama katika maeneo kama vile 'Notre Dame'na Mtakatifu Louis, na kufikia hadi Kusini-magharibi na California. Operesheni hiyo iliagizwa na kuidhinishwa hapo awali na Papa Francisko, huku mapato yakienda kwa maskini, hasa watoto ambao ni wahanga wa vita ulimwenguni kote.
"Utakatifu wa Kikristo," aliandika Papa Leo XIV katika Dilexi te, Wosia wa Kitume kuhusu upendo kwa maskini, "mara nyingi hustawi katika maeneo yaliyosahaulika na kujeruhiwa zaidi ya wanadamu. Maskini zaidi ya maskini huchukua nafasi maalum katika moyo wa Mungu. Wao ndio wapendwa wa Injili, warithi wa Ufalme. Ni ndani yao ambapo Kristo anaendelea kuteseka na kufufuka tena. Ni ndani yao ambapo Kanisa hugundua upya wito wa kufichua ukweli wake halisi zaidi." Hili ndio agizo ambalo Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo hutekeleza kila wakati kwa kujitolea sana.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here