Kard.Parolin:Ningesema kwa Trump na Israeli waache,ongezeko la uchumi liko karibu!
Salvatore Cernuzio na Tiziana Campisi-Roma.
Kama angejikuta ana kwa ana na Rais wa Marekani Donald Trump, Katibu Mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin angemwambia "akomeshe haraka iwezekanavyo kwa sababu hatari halisi ya kuongezeka kwa uchumi iko juu yetu. Ningesema tuiache Lebanon..." Kardinali alisema ujumbe huo huo unapaswa pia "kuelekezwa kwa Waisraeli" ili wajaribu kweli "kutatua matatizo ambayo yanaweza kuwepo, au ambayo wanaamini yapo, kupitia njia za amani za diplomasia na mazungumzo."
Kardinali alishirikisha mawazo yake katika uwanja wa kimataifa huku akijibu maswali ya waandishi wa habari katika Baraza la Manaibu, wa Italia kando ya uwasilishaji wa Kitabu cha Papa Leo XIV.
"Mnasema mimi ni nani? Mimi ni mwana wa Mtakatifu Agostino," ndicho kitabu kilichochapishwa na Cantagalli na kilichoandikwa na mtaalamu wa Vatican Ignazio Ingrao na Padre Giuseppe Pagano(OSA). Na Kardinali alizungumza hasa kuhusu Papa Leo XIV kwa waandishi wa habari waliomuuliza jinsi ilivyo kufanya kazi pamoja na Papa wa kwanza wa Marekani katika historia: "Ni rahisi sana," alielezea. "Kuna mazungumzo mazuri, mazungumzo mazuri. Anasikiliza sana, na tuna uhusiano mzuri."
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku bonyeza hapa: Just click here.