Vatican kuhusu upunguzaji wa silaha:amani haiwezi kupatikana kupitia kuzuia pekee
Vatican News.
Katika hotuba ya Monsinyo Daniel Pacho, Katibu Msaidizi wa Vatican wa Sekta ya Mashirika Mbalimbali ya Kitengo cha Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa, alihutubia katika Kitengo cha Ngazi ya Juu cha Kikako cha 61 cha Baraza kwa ajili ya Haki za kibinadamu cha Umoja wa Mataifa na katika kikao cha 2026 cha Mkutano wa Kupunguza Silaha, tarehe 25 februari 2026 huko Geneva, Uswiss. Pacho alisema kuwa “miaka ishirini imepita tangu kuanzishwa kwa Baraza hili la Haki za Binadamu. Tangu wakati huo, dunia imebadilika sana na ushirikiano wa pande nyingi umedhoofika.”
Mpango wa haki za binadamu kwa sasa unakabiliwa na mgogoro wa uaminifu
"Diplomasia inayokuza mazungumzo na kutafuta makubaliano miongoni mwa pande zote inabadilishwa na diplomasia inayotegemea nguvu, na watu binafsi au vikundi vya washirika.” Hata hivyo, katikati ya hali hii inayobadilika, haki za binadamu zinabaki kuwa msingi wa jamii yoyote inayostawi, ikitoa matumaini na kukataa dharau kwa nyingine, ukatili, na dhuluma. Hata hivyo, mpango wa haki za binadamu kwa sasa unakabiliwa na mgogoro wa uaminifu. Kujitenga na mifumo ya pande nyingi na baadhi ya Mataifa kunatia wasiwasi hasa, kama vile mmomonyoko wa maana katika mfumo wa pande nyingi.
Vatican inabainisha kwamba “uaminifu huharibika wakati kanuni za msingi za mfumo, kama vile Azimio la Haki za Binadamu la Ulimwengu, Maagano na Mikataba ya Haki za Binadamu, hazizingatiwi tena kama "lugha ya pamoja" na "ajenda ya pamoja" lakini badala yake zinatafsiriwa upya au kuidhinishwa kwa kuchagua.” Mabadiliko haya yana uwezo wa kuwa na matokeo makubwa, ikiwa ni pamoja na kuvunjika kwa mazungumzo na uaminifu, pamoja na ugawaji mbaya wa nishati na rasilimali muhimu ambazo zinaweza kutumika kushughulikia sababu za msingi za mateso duniani. Suala hili linazidishwa zaidi na kuenea kwa kinachoitwa "haki mpya".
Tunaona 'mzunguko mfupi' halisi wa haki za binadamu
Mons. Pacho alisisitiza kwamba ni dhahiri kwamba kuna kitendawili kinachozingatiwa, ambapo haki za msingi zinazuiliwa chini ya kivuli cha haki hizi zinazoitwa mpya. Hakika, kama Papa Leo XIV anavyothibitisha, "katika muktadha wa sasa, tunaona 'mzunguko mfupi' halisi wa haki za binadamu. Haki ya uhuru wa kujieleza, uhuru wa dhamiri, uhuru wa kidini na hata haki ya kuishi inazuiliwa kwa jina la haki zingine zinazoitwa mpya, na matokeo yake ni kwamba mfumo wenyewe wa haki za binadamu unapoteza nguvu zake na kuunda nafasi ya nguvu na ukandamizaji.”
Ulinzi wa haki ya kuishi ndiyo msingi muhimu wa kila haki
Katiaka hotuba hiyo alisema kuwa hili hutokea wakati kila haki inakuwa ya kujirejelea, na hasa inapotenganishwa na uhalisia, asili na ukweli." "Ulinzi wa haki ya kuishi ndio msingi muhimu wa kila haki nyingine ya binadamu." Ahadi hii imejengwa juu ya ulinzi wa hadhi isiyoweza kuondolewa ya kila mtu, kuanzia wakati wa kutungwa mimba hadi kifo cha asili. Ahadi hii inaonekana wazi katika ulinzi wa familia, jengo la msingi zaidi la jamii, ambapo maisha ya binadamu yanakuzwa na kuendelezwa.
Leo hii mateso yanaendelea dhidi ya Wakristo,yakiathiri zaidi ya waamini milioni 380
Vatican aidha inabainisha kwamba ni muhimu sana kukabiliana na tabia ya wasiwasi ndani ya mfumo wa kimataifa ya kupuuza na kuitenga taasisi ya familia, tukizingatia kwamba "kama familia inavyokwenda, ndivyo ulimwengu wote unavyokwenda". Pia ni muhimu kuhakikisha kikamilifu haki ya uhuru wa dini au imani, "haki ya kwanza ya binadamu [ambayo] inaonesha ukweli wa msingi zaidi wa mwanadamu". Mojawapo ya migogoro iliyoenea zaidi katika ulimwengu wa leo ni mateso yanayoendelea dhidi ya Wakristo, yanayoathiri zaidi ya waamini milioni 380.
Ni muhimu kurudi kwenye njia pekee yenye uwezo wa kuzalisha amani
Mwakilishi wa Vatican alibainisha kuwa hali hii mbaya imezidi kuwa mbaya mwaka 2025 kutokana na sababu zinazozidisha migogoro na itikadi kali. Zaidi ya hayo, ni muhimu kushughulikia jambo la "mateso ya adabu" linaloenea katika jamii za Magharibi, ambapo waamini wanazidi kuwekewa vikwazo katika kuishi na kutangaza Injili, hasa linapokuja suala la kulinda uhai kuanzia mimba hadi mwisho wake wa asili, familia, au wahamiaji, chini ya kivuli cha "uvumilivu." Kwa kuhitimisha Monsinyo Pacho alisema kuwa: “ ili kulinda maendeleo ya miongo minane iliyopita, ambayo yamepatikana kwa bidii tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa, ni muhimu kurudi kwenye njia pekee yenye uwezo wa kuzalisha amani: mazungumzo yaliyojengwa imara katika hadhi isiyoweza kuondolewa ya mwanadamu kutoka kwa Mungu.”
Asante kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here