Tafuta

2024.12.06: Askofu Mkuu Gallagher,Katibu wa Vatican wa  Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa akihutubia OSCE. 2024.12.06: Askofu Mkuu Gallagher,Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa akihutubia OSCE. 

Ask.Mkuu Gallagher:Pande zote zitende haraka kwa mazungumzo ya utafutaji wa amani

Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa alihutubia mkutano wa 1554 wa Baraza la Kudumu la OSCE mnamo Februari 24,akihimiza wenye nafasi za juu za umma kuweka kipaumbele kusitishwa kwa shughuli za kibinadamu mara moja,pamoja na kuendelea kwa ushiriki wa kidiplomasia. Mazungumzo lazima yachochewe na utafutaji wa dhati wa njia zinazoongoza kuelekea amani.

Vatican News.

Katika hotuba yake kwenye kikao cha 1554 cha Baraza la Kudumu la Shirika la Usalama na Ushirikiano Ulaya (OSCE) , tarehe 24 Februari 2026, huko Vienna, Austria, Askofu Mkuu Pual Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Nchi na Mashirika ya Kimataifa, alibainisha kuwa “kila vita inawakilisha kushindwa kimaadili na kibinadamu. Alisisitiza hayo hasa katika maadhimisho ya miaka minne ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, huku akitoa wito wa pande zote kuonyesha ujasiri wa kisiasa unaohitajika ili kuanzisha na kudumisha njia za kidiplomasia za dhati na jumuishi zinazolenga amani ya haki na ya kudumu.

“Kila vita inawakilishwa kushindwa kwa maadili na kibinadamu”

Akianza hotuba yake Askofu Mkuu Gallagher alisema, “Ni kwa moyo mzito tunapoadhimisha mwaka wa nne tangu kuanza kwa vita vya kusikitisha dhidi ya Ukraine. Kila vita inawakilisha kushindwa kimaadili na kibinadamu. Zaidi ya kanuni ya ulinzi halali, mantiki kama hiyo ya makabiliano sasa inatawala siasa za kimataifa, ikizidisha ukosefu wa utulivu na kutotabirika siku hadi siku”, na kulazimisha watu kuishi katika hali ya hofu ya kila mara.

Amani ipo, inataka kukaa ndani yetu”

Kama Papa Leo XIV alivyotukumbusha, aliongeza “Amani ipo; inataka kukaa ndani yetu. Kazi si kuiunda, bali ni kuikaribisha, na kuiruhusu ipoteze silaha.” Katika roho hii, Vatican inawasihi pande zote zenye mzozo kuonesha ujasiri muhimu wa kisiasa ili kuanzisha na kudumisha njia za kidiplomasia za dhati na jumuishi zinazolenga amani ya haki na ya kudumu. Hatua thabiti lazima zichukuliwe. Wale waliopewa jukumu kubwa zaidi la umma lazima watoe kipaumbele kwa kusimamishwa mara moja kwa kibinadamu pamoja na ushiriki endelevu wa kidiplomasia, kwa lengo la kutafsiri nia njema kuwa mipango inayoweza kuthibitishwa na ya kudumu ya amani.”

"Mazungumzo yaegemee uaminifu"

“Mazungumzo haya lazima yategemee uaminifu katika mazungumzo na utimilifu wa uaminifu wa majukumu,” alisema Askofu Mkuu Gallgher. Katika suala hilo, Vatican inaamini kwamba OSCE inaweza kuchukua jukumu maalum katika kuwezesha mazungumzo, kujenga kujiamini, na kutekeleza hatua zinazoonekana zinazopunguza mateso ya wanadamu na kurejesha usalama, na iko tayari kuunga mkono mipango yoyote ya kidiplomasia inayoweka mwanadamu na kupunguza mateso katikati ya juhudi zao.

"Hali hii haiwezi kutegemea maslahi ya kijeshi na kimkakati"

Zaidi ya hayo, aliomba aruhusiwe  kutoa wasiwasi wa Papa Leo XIV kuhusu umuhimu wa kufuata sheria za kimataifa za kibinadamu. Hili haliwezi kutegemea hali tu au maslahi ya kijeshi na kimkakati. Hakika, "Sheria ya kibinadamu, pamoja na kuhakikisha kiwango cha chini cha ubinadamu wakati wa uharibifu wa vita, ni ahadi ambayo Mataifa yameitoa. Sheria kama hiyo lazima ishinde matarajio ya wapiganaji kila wakati, ili kupunguza athari mbaya za vita, pia kwa lengo la ujenzi upya." Wakati huo huo, huku ikitaja utakatifu wa maisha na hadhi ya binadamu, Vatican inatoa wito kwa pande zote zenye migongano kutenda kwa haraka na huruma na kujitahidi kuwa na "mazungumzo yanayochochewa na utafutaji wa dhati wa njia zinazoelekea kwenye amani,” alihitimisha.

Asante kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here

26 Februari 2026, 16:01