Tafuta

Kanisa la Mama Yetu wa Arabia huko Kuwait. Kanisa la Mama Yetu wa Arabia huko Kuwait.  (Copyright (c) 2024 demesafrankc/Shutterstock. No use without permission.)

Ziara ya Kardinali Parolin huko Kuwait Januari 15 na 16

Katibu Mkuu wa Vatican atasafiri kwenda nchi ya Asia akiwa na mpango unaojumuisha ziara za Msikiti Mkuu na Jumba la Makumbusho la Vitu vya Kale vya Kiislamu.Misa pia imepangwa katika Kanisa Kuu la Familia Takatifu kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 65 ya kuwekwa wakfu kwake na katika Basilika Ndogo ya Mama Yetu wa Arabia huko Ahmadi,wakati wa kuinuliwa kwake kuwa Basilika Ndogo ya Vikariate ya Kitume ya Arabia Kaskazini.

Vatican News

Katibu Mkuu wa  Vatican,  Kardinali Pietro Parolin atatembelea Kuwait kuanzia tarehe 15 na 16 Januari 2026. Kulingana na programu iliyochapishwa na akaunti ya X ya Sekretarieti ya Vatican @TerzaLoggia, Kardinali baada ya ziara za heshima kwa mamlaka za kiraia mahalia siku ya Alhamisi Januari 15, atatembelea Msikiti Mkuu na Dar al Athar al Islamiyyah (Jumba la Makumbusho la Vitu vya Kale vya Kiislamu). Kisha atakutana na mapadre  na watawa wa kike na kiume  katika Kanisa Kuu la Familia Takatifu.

Mikutano na Sherehe

Programu hiyo pia inajumuisha Misa mbili: ya kwanza, pia Alhamisi hiyo, katika Kanisa Kuu la Familia Takatifu kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 65 ya kuwekwa wakfu kwa Kanisa hilo.

Siku ya Ijumaa Januari 16

Siku ya pili, Ijumaa tarehe 16 Januari, ataadhimisha katika Basilika Ndogo ya Mama Yetu wa Arabia huko Ahmadi, wakati wa kuinuliwa kwake kuwa Basilika Ndogo ya Vikariate ya Kitume ya Arabia Kaskazini, ambayo inajumuisha, pamoja na Kuwait, Bahrain, Qatar na Saudi Arabia.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here

 

14 Januari 2026, 17:28