Papa amteua Alí Herrera kuwa Makamu wa Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu!
Vatican News
Papa Leo XIV tarehe 15 Januari 2026, alimteua Askofu Luis Manuel Alí Herrera, ambaye hadi uteuzi alikuwa katibu wa Tume ya Kipapa ya Ulinzi wa Watoto, kuwa Makamu Mkuu wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu(Santa Maria Maggiore).
Awali alikuwa Askofu msaidizi mstaafu wa Bogotá nchini Colombia, na mwanasaikolojia anayejulikana kwa kujitolea kwake katika ulinzi wa watoto, Herrera ambaye aliteuliwa kuwa katibu wa Tume ya Ulinzi wa Watoto na Watu Wazima Walio katika Mazingira hatarishi mnamo Machi 2024. Ataendelea na wadhifa huu baada ya uteuzi wake kuwa Makamu Mkuu tarehe 15 Januari 2026.
Katika Kanisa Kuu la Liberia, yaani la Mtakatifu Maria Mkuu, Askofu Alí Herrera atashirikiana na Kardinali Rolandas Makrickas, Mkuu wa Kanisa Kuu hilo.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here