Tafuta

Jumba la Mahakama ya Kitume mjini Vatican. Jumba la Mahakama ya Kitume mjini Vatican. 

Kesi ya Vatican:Mahakama Kuu ya Rufaa yakubali kutofanya uamuzi

Mahakama Kuu ya Rufaa ya Vatican iliamua kwa amri mbili kuhusu rufaa zilizowasilishwa na Mtetezi wa Hakimu Alessandro Diddi,ikikubali tamko lake la kutohudhuria katika Kesi kuhusu usimamizi wa fedha za Vatican na kuthibitisha kutokubalika rufaa yake dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Rufaa wa mwezi Septemba 25 iliyopita.

Na Salvatore Cernuzio – Vatican.

Mahakama ya ya Rufaa ya Jiji la Vatican imekubali tamko lililowasilishwa na Mtetezi wa Haki, Alessandro Diddi, la kujiepusha na mchakato wa rufaa kuhusu usimamizi wa fedha za Kiti kitakatifu. Na ilithibitisha "kutokubalika" kwa rufaa ambayo Diddi mwenyewe alikuwa ameiwasilisha kwa Mahakama ya Rufaa ya Vatican, ambapo ngazi ya pili ya kesi za kimahakama inaendelea. Kesi hiyo, iliyoanza tarehe 22 Septemba 2025, baada ya muda mrefu uliowekwa na Askofu Alejandro Arellano Cedillo, itaendelea tena kunako Februari 3.

Hii hasa zaidi, kama ilivyoripotiwa katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Habari ya Kiti Kitakatifu, Mahakama ya Rufaa, iliyoundwa na majaji wanne, Makardinali Farrell, Rais, Lojudice, Zuppi, na Gambetti, ilitoa maamuzi mawili kuhusu rufaa zilizowasilishwa na Mtetezi wa Haki. "Katika kesi moja," inasomeka, "ikikubali tamko la kujiepusha katika kesi" na, katika nyingine, "ikithibitisha kutokubalika" kwa rufaa ya mtetezi iliyotangazwa na Mahakama ya Rufaa.

Kukataliwa

Kikao cha kwanza cha kesi ya rufaa kilihusiana na uuzaji wa jengo la London na masuala mengine ya kifedha kilianza Septemba huku washtakiwa wanne wakiwasilisha ombi la kumkataa Diddi (ambaye aliwakilisha upande wa mashtaka katika kesi ya kwanza na ya pili). Mawakili wa utetezi walitegemea hoja hii kwa kile walichokielezea kama ushiriki wa Diddi katika mazungumzo ya WhatsApp na watu walio nje ya uchunguzi, ambayo, hata hivyo, yalikuwa yamemshawishi mmoja wa mashahidi, na kudhoofisha hadhi ya "mtu wa tatu" na utafutaji wa "ukweli wa ukweli." Hoja hiyo ilitangazwa "kukubalika" na Mahakama na kupelekwa kwa Mahakama Kuu ya Cassation, ambayo ilitakiwa kutoa uamuzi kuhusu jambo hilo. Na hivyo ndivyo ilivyofanya leo, baada ya mikutano iliyofanyika wiki iliyopita.

Rufaa

Kuhusu suala lingine, Diddi alikuwa amewasilisha rufaa dhidi ya kuachiliwa huru kadhaa kuamuliwa katika uamuzi wa kesi ya kwanza uliotolewa na Mahakama ya Vatican mnamo Desemba 2024. Mawakili wa utetezi walikuwa wamepinga ombi la mtetezi, wakipinga masuala hayo  hata ucheleweshaji wa muda. Mnamo Septemba 25, Mahakama ya Rufaa ilikubali ombi la upande wa utetezi, na kutupilia mbali rufaa ya Diddi. Diddi, naye, alikata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Rufaa kwa Mahakama Kuu ya Rufaa. Hata hivyo, kama ilivyotangazwa tena, Mahakama Kuu  ilitangaza rufaa hiyo  kuwa "haikubaliki."

 

13 Januari 2026, 11:21