Tafuta

2025.10.25 Bwana  Nawaf Abdallah Salim Salam, Waziri Mkuu wa Lebanon. 2025.10.25 Bwana Nawaf Abdallah Salim Salam, Waziri Mkuu wa Lebanon.  (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Lebanon

Papa Leo XIV,alikutana tarehe 25 Oktoba na Waziri Mkuu na Makamu Waziri wa Lebanon,katika matarajio ya Ziara yake ya kitume kuanzia tarehe 30 Novemba hadi 2 Desmba 2025.

Vatican News

Katika matarajio ya  ziara ijayo ya Kitume ya Papa Leo XIV ya kwenda nchini Lebanon, iliyopangwa kufanyika Novemba 30 hadi tarehe 2 Desemba 2025, Jumamosi asubuhi tarehe 25 Oktoba 2025, Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana na  Waziri Mkuu wa Lebanon, Nawaf Salam akiambatana na Naibu Waziri Mkuu Tarek Mitri katika Mkutano uliyofanyika mjini Vatican.

Wakati wa kubadilishana zawadi
Wakati wa kubadilishana zawadi   (@VATICAN MEDIA)

Baadaye, alikutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, akifuatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa  Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Waziri Mkuu wa Lebanon akiwa na Katibu Mkuu wa Vatican
Waziri Mkuu wa Lebanon akiwa na Katibu Mkuu wa Vatican   (@VATICAN MEDIA)

Wakati wa majadiliano, kulingana na taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Vatican, "matarajio ya pamoja ya Ziara ya Kitume ya Baba Mtakatifu yalioneshwa." Baadaye, "mkutano huo ulitambua matumaini yaliyowekwa na watu wa Lebanon katika mchakato wa mageuzi na utulivu wa nchi hiyo na kupanuka hadi muktadha wa kikanda, kwa matumaini ya pamoja kwamba utulivu kamili wa Levant nzima utapatikana hivi karibuni."

Mkutano katika sekretarieti ya Vatican.
Mkutano katika sekretarieti ya Vatican.   (@VATICAN MEDIA)
Papa na waziri Mkuu wa Lebanon

 

25 Oktoba 2025, 15:56