Tafuta

2025.10.20 Papa na waziri Mkuu wa Armenia Bwana Nikol Pashinyan. 2025.10.20 Papa na waziri Mkuu wa Armenia Bwana Nikol Pashinyan.  (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Armenia

Papa Leo XIV alikutana katika Jumba la Kituma na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Armenia Nikol Pashinyan,Oktoba 20.Katika mazungumzo na Sekretarieti ya Vatican walijikita juu ya maisha ya Kanisa katika Nchi,ya utamaduni wa kale wa Kikristo, na umuhimu wa amani ya kudumu huko Caucasus kusini.

Vatican News

Baba Mtakatifu  Leo XIV tarehe 20 Oktoba 2025 alikutana na Bwana Nikol Pashinyan, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Armenia katika Jumba la  Kitume. Baadaye Pashinyan alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu  Mkuu wa Vatican,  akiambatana  na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Papa Leo XIV alikutana na Waziri Mkuu wa Armenia
Papa Leo XIV alikutana na Waziri Mkuu wa Armenia   (@VATICAN MEDIA)
Waziri Mkuu wa Armenia wakati wa kubadilishana zawadi na Papa
Waziri Mkuu wa Armenia wakati wa kubadilishana zawadi na Papa   (@VATICAN MEDIA)

Mazungumzo katika Sekretarieti ya Nchi

"Wakati wa majadiliano ya kindani katika Sekretarieti ya Vatican, katika taarifa kutoka Ofisi ya Habari inasema, "kuridhika kulioneshwa kwa uhusiano mzuri kati ya Vatican na Armenia, nchi yenye utamaduni wa kale wa Kikristo, na vipengele fulani vya maisha ya Kanisa Katoliki nchini humo vilioneshwa." "Wakati huo huo," taarifa hiyo inaendelea, "tahadhari ilitolewa kwa masuala mengine ya maslahi ya pande zote, hasa haja ya amani ya utulivu na ya kudumu katika Caucasus Kusini."

Waziri Mkuu wa Armenia alikutana baadaye na Katibu Mkuu wa Vatican
Waziri Mkuu wa Armenia alikutana baadaye na Katibu Mkuu wa Vatican   (@Vatican Media)
22 Oktoba 2025, 18:30