Tafuta

2025.10.27 Papa na Waziri Mkuu wa Hungaria Bwana Viktor Orban. 2025.10.27 Papa na Waziri Mkuu wa Hungaria Bwana Viktor Orban.  (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Rais wa Hungaria:mahusino mema baina ya Vatican na Hungaria

Papa Leo alikutana na Waziri Mkuu wa Hungaria ambapo mara baada ya Mkutano huo alikutana na Sekretarieti ya Vatican.Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi za vyombo vya habari,Vaticam imebanisha kuwa sehemu kubwa ya mazungumzo yap ni pamoja na masuala ya Ulaya kwa namna ya pekee umakini wa mgogoro wa Ukraine na hali halisi ya Mashariki ya Kati.”

Vatican News

Baba Mtakatifu Leo XIV, Jumatatu tarehe 27 Oktoba 2025 alikutana na Waziri Mkuu wa Hungaria, Bwana Viktor Orbán, ambapo mara baada ya mkutano huo alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican akiambatana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa Mahusiano na nchi na Mashirikia ya Kimataifa.

Waziri Mkuu wa Hungaria na mkewe pamoja na Papa
Waziri Mkuu wa Hungaria na mkewe pamoja na Papa   (@VATICAN MEDIA)

Katika mazungumzo yao, kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya habari Vatican, walionesha uhusiano thabiti kati yao na kupongeza jitihada za Kanisa Katoliki katika kuhamasisha  maendeleo kijamii na ustwi wa Jumuiya ya Hungaria, kwa namna ya pekee umakini katika nafasi ya familia, mafunzo na wakati ujao wa vijana ikiwa ni pamoja na umuhimu wa kulinda jumumuiya za kikristo zilizo katika mazingira magumu.”

Waziri Mkuu wa Hungaria na Kardinali Parolin
Waziri Mkuu wa Hungaria na Kardinali Parolin   (@Vatican Media)

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi za vyombo vya habari, Vaticam imebanisha kuwa sehemu kubwa ya mazungumzo hayo ilipewa “masuala ya Ulaya kwa namna ya pekee umakini wa mgogoro wa Ukraine na hali halisi ya Mashariki ya Kati.”

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Hungaria
27 Oktoba 2025, 15:38