Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Allegro con fuoco
Ratiba Podcast
Miaka 20 ya Kifo cha Mtakatifu Yohane Paulo II kilichotokea tarehe 2 Aprili 20005. Miaka 20 ya Kifo cha Mtakatifu Yohane Paulo II kilichotokea tarehe 2 Aprili 20005. 

Kard.Parolin ataadhimisha misa katika kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Papa Yohane Paulo II

Katika kumbukizi ya miaka 20 tangu Papa Yohane Paulo II aliaga dunia,Jumatano tarehe 2 Aprili saa 9.00 alasiri masaa ya Ulaya,Katibu wa Vatican atongoza ibada ya Misa Takatifu.Katika altare atakuwapo hata Kardinali Stanisław Dziwisz,ambaye Papa Francisko alimtumia Barua yake kwa kumhakikishia baraka zake kwa washiriki wote.

Vatican News

Zaidi ya mwezi mmoja uliopita, tarehe 12 Februari iliyopita, Papa Francisko alituma barua Kardinali Stanisław Dziwisz, ambapo aliwahakikishia washiriki wa maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 20 ya kifo cha Mtakatifu Yohane Paulo II. “Nawatakia kila mtu Mwaka mtulivu wa Jubilei yenye tumaini,” aliandika Papa Francisko na, nikiomba maombezi ya Bikira Mbarikiwa na Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili, ninawabariki kwa moyo wote ninyi na wote watakaoshiriki katika Sherehe hiyo Aprili 2 ijayo.”

Misa na Mkesha wa tarehe 2 Aprili  

Kardinali Dziwisz atakuwa katika Kanisa kuu la Vatican wakati tarehe 2 Aprili 2025 saa 9:00 alasiri, Kardinali Pietro Parolin Katibu wa Vatican atakuwa juu ya madhabahu kuongoza maadhimisho ya Liturujia ya Ekaristi. Kushiriki Misa hiyo itakuwa wazi kwa wote, bila kuhitaji pasi yoyote. Siku hiyo hiyo, majira ya saa 3.00 usiku masaa ya Ulaya, kutakuwa na maombi kwa lugha ya Kipoland na Kiitaliano katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, yatakayoongozwa na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Poland, Askofu Mkuu Tadeusz Wojda, ambaye pia atakuwa miongoni mwa wakonselebranti wa Liturujia ya alasiri.

Kardinali Reina:“zawadi kuu" ya maisha ya Papa Wojtyla

Katika siku za hivi karibuni, katika barua kwa mapadre, watawa, jumuiya na waamini wa Jimbo la Roma, Kardinali Baldassare Reina alifafanua kuwa maisha ya Mtakatifu Yohane Paulo II ni kama zawadi kuu pia, kwa huduma yake ya kichungaji katika jimbo letu,  akiwaalika kila mtu kushiriki katika hafla hiyo.

Ikumbukwe Papa Yohane Paulo II alizaliwa mnamo tarehe 18  Mei 1920, huko Wadowice, Poland. Katika ujana wake, Wojtyła alishiriki katika uigizaji wa jukwaa. Alihitimu kwa alama bora zaidi katika shule ya Sekondari ya wavulana wote huko Wadowice, nchini Poland, mnamo mwaka 1938, baada ya muda mfupi Vita vya Pili vya Ulimwengu vilipozuka. Alichaguliwa kuwa Kharifa wa Mtume Petto kuanzia mwaka  1978 hadi kifo chake mnamo mwaka wa 2005 akiwa na umri wa miaka 84, katika Jumba la Kitume mjini Vatican.

 

01 Aprili 2025, 13:32
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031