Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
PROGRAMU YA KISWAHILI
Ratiba Podcast
12 ya upapa wa Papa Francisko (13 Machi 2013  -  13 Machi 2025). 12 ya upapa wa Papa Francisko (13 Machi 2013 - 13 Machi 2025).  

Sauti ya Baba Mtakatifu Francisko na Majisterio ya udhaifu

Mhariri Mkuu wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano,Dk.Andrea Tornielli,anaandika tahariri kuhusu miaka 12 ya Upapa wa Baba Mtakatifu kwamba:“Katika maadhimisho ya miaka kumi na mbili ya kuchaguliwa kwake kuwa papa,Papa Francisko anaendelea kupata nafuu katika hospitali ya Gemelli,Roma.”

Andrea Tornielli

Mwaka huu, maadhimisho ya miaka kumi na mbili ya upapa wake yanaangukia wakati maalum kwa Papa Francisko, ambaye amekuwa akiishi katika chumba chake cha hospitali kwenye ghorofa ya kumi ya Hospitali ya Gemelli kwa karibu mwezi mmoja. Habari zinazotoka kwenye taarifa za  karibuni za matibabu ni za kutia moyo, utabiri wake hauhifadhi tena na tunatumaini kuwa ataweza kurejea Vatican hivi karibuni.

Bado, kile ambacho Papa anapitia wakati huu bila shaka kinafanya ukumbusho huu wa mwanzo wa upapa wake wa kuwa wa kawaida sana. Mwaka uleule ambao umeona safari ndefu zaidi kati ya mabara kwa Papa Francisko (kwenda Indonesia, Papua New Guinea, Timor ya Mashariki na Singapore…); hitimisho la Sinodi ya kisinodi; na kufunguliwa kwa Mlango Mtakatifu uliozindua Jubilei, sasa kunashuhudia kifungu hiki maralum.

Mrithi wa Mtakatifu Petro, mgonjwa kati ya wagonjwa, anateseka na kuomba amani, akisindikizwa na kwaya ya sala za watu wengi duniani kote. Yeye, ambaye katika miaka hii kumi na miwili hajawahi kuhitimisha mkutano, katekesi au sala ya Malaika Malaika bila maneno ya: “Tafadhali msisahau kuniombea”, leo hii anahisi kukumbatiwa na waamini wengi na wasioamini wanaomjali sana. Inadhihirisha kwani: ni wakati wa kuzingatia asili ya Kanisa na utume wa Askofu wa Roma, ambao ni tofauti sana na ule wa mkuu wa shirika la kimataifa.

Miaka kumi na miwili iliyopita, Kardinali Bergoglio wa wakati huo alihutubia Makutano Mkuu, akinukuu maoni ya Henri De Lubac kwamba: "uovu mbaya zaidi" ambao Kanisa linaweza kuingia ni "ulimwengu wa kiroho:" Hatari ya Kanisa ambalo "linajiamini kuwa lina nuru yake yenyewe", ambalo linategemea nguvu zake lenyewe, mikakati yake yenyewe, ufanisi wake wenyewe, na hivyo kuacha kuwa "fumbo la mwezi", yaani, kutoakisi tena nuru ya Mwingine, kutoishi tena na kutenda kwa neema  tu ya Yule aliyesema: “Pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.”

Tukikumbuka maneno hayo kwa mara nyingine tena, leo hii, tunatazama kwa upendo na matumaini kwenye madirisha ya orofa ya kumi ya Hospitali ya Gemelli. Tunamshukuru Baba Mtakatifu Francisko kwa uzoefu  huu wa udhaifu, kwa sauti yake hiyo dhaifu ambayo bado imejiunga na Rozari kwenye Uwanja wa Mtakatifu Petro,  katika siku za hivi karibuni, kwa sauti tete inayoendelea kusihi amani na si vita, mazungumzo na si uonevu, huruma na si kutojali. Heri ya kumbukumbu ya miaka, Papa Francisko! Bado tunahitaji sauti yako sana!

13 Machi 2025, 10:31
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031