Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Messa di Requiem per soli, coro e orchestra [ Scritto per la morte di Bellini; prima esec. Bergamo 1870 ]
Ratiba Podcast
Kardinali Parolin akiwa pembezoni mwa hafla iliyoandaliwa na Ubalozi wa Morocco mjini Vatican. Kardinali Parolin akiwa pembezoni mwa hafla iliyoandaliwa na Ubalozi wa Morocco mjini Vatican.  (ANSA)

Kard.Parolin:Kupokonya silaha na kudhibitiwa kunahitajika,amani ya haki na kudumu nchini Ukraine

Kardinali Katibu wa Vatican ambaye alizungumza pembeni mwa toleo la kwanza la “Meza ya Ramadhan-Iftar,”alisisitiza umuhimu wa kuanza mchakato unaomaliza mzozo unaoendelea Ulaya Mashariki, kuepusha “masharti ambayo yanazuia mazungumzo.”

Vatican News

Kupokonya silaha, vita nchini Ukraine, hali ya Papa Francisko zilikuwa ni mada kadhaa zilizoguswa na Kardinali Pietro Parolin Katibu wa Vatican tarehe 17 Machi 2025  mjini Roma kando ya toleo la kwanza la “ Meza ya Ramadan – Iftar,” mpango uliohamasishwa na Ubalozi wa Morocco anayewakilisha mjini Vatican, na shirika la Klabu ya Mawasiliano ya Kimataifa ya Vyombo vya Habari - MICC, ambapo Katibu wa Vatican alipokea tuzo ya “Nyuso zilizofichika za  Mazungumzo" kutoka kwa Balozi wa Morocco, Rajae Naji El Mekkaoui,

Kardinali huyo alikumbuka kuwa Vatican imekuwa na sera ya wazi kuhusu kuweka silaha tena tangu Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, "yaani, kusisitiza katika ngazi ya kimataifa kwamba kuwe na upokonyaji silaha kwa ujumla na kudhibitiwa. Kwa hivyo hatuwezi kufurahishwa na mwelekeo wa  mambo yanavyokwenda." Kuhusu uwezekano wa mapatano kati ya Urusi na Ukraine Kardinali Parolin alitumaini "kwamba hakuna masharti yoyote yatakayowekwa ili kuzuia kuanza kwa mazungumzo", akimaanisha ukweli kwamba Moscow imeweka mipaka "katika suala la kuthibitisha utiifu wa makubaliano hayo. Lakini mchakato huu uanze hata hivyo: ukizingatiwa kwamba Ukraine hatimaye iko tayari, basi kuwe na nia ya upande mwingine kuanzisha usitishaji vita ambao unapaswa kudumu kwa siku 30.”

Hatua inayofuata, anatumaini Kardinali, ni kuanzisha mazungumzo kutoka hapo ambayo yanaweza kukomesha vita na kuanzisha amani ya haki na ya kudumu ambayo tumeitarajia.” Kisha Kardinali Parolin aliulizwa na waandishi wa habari kuhusu afya ya Papa, akisisitiza kwamba taarifa za matibabu zinatuambia ni nini hasa masharti ya Papa. “Mimi  nilimwoma juma moja lililopita  basi sikupata nafasi ya kumuona tena kama ilivyokuwa mara ya kwanza. Lakini hii ni tathmini ya nje, basi kwa wengine tunapaswa kushikamana na kile ambacho madaktari wanatuambia.” Katika mikutano hiyo, Katibu wa Vatican alifafanua, “tunawasilisha kwake masuala na matatizo ambayo yanahitaji ufumbuzi na Papa anatoa maoni yake” Hatimaye , alipoulizwa kama kulikuwa na mazungumzo yoyote ya uwezekano wa kujiuzulu kwa Francisko, Kardinali Parolin alijibu: “Hakuna kabisa.”

Kardinali Parolin
18 Machi 2025, 12:19
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031