Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Presto
Ratiba Podcast
2024.11.24 Santa Messa nella Solennita' di Cristo Re

Jubilei ya Wamisionari wa Huruma:Zaidi ya Mapadre 500 kutoka mabara yote!

Tukio la Jubilei kuu ya sita litafanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Machi 2025 kwa kushirikisha mapadre wamisionari wa huruma kutoka pande zote za dunia,wakisindikizwa na familia zao na washiriki.Ujumbe ulioandikwa unatarajiwa kutoka kwa Papa Francisko ambaye bado anaendelea kupata nafuu na hataweza kushiriki.

Vatican News

Kuanzia Italia, Marekani, Poland, Brazil, Hispania, Ufaransa, Mexico, Ujerumani, Slovakia, Ufilipino, Bangladesh, Ukrane, Colombia, India, ni baadhi tu ya nchi ambazo wamisionari wa Huruma  wapatao 500 wanatoka, kuanzia Ijumaa,Machi 28, hadi Dominika  waweza kuishi Uzoefu wa Jubilei yao, ambayo ni ya sita kati ya matukio makuu yaliyoratibiwa kwa Mwaka Mtakatifu Mtakatifu uliowekwa wakfu kwa ajili ya matumaini. Papa Francisko ambaye alirejea Nyumbani, Mtakatifu Marta, mjini Vatican baada ya kulazwa hospitalini kwa zaidi ya mwezi mmoja huko Gemelli, hataweza kushiriki lakini atatuma ujumbe wa maandishi.

Idadi ya wamsionari wa huruma inaongezeka

Idadi ya Wamisionari wa Huruma, ambayo huduma yao maaalum  ilianzishwa na Papa wakati wa kuadhimisha Mwaka Mtakatifu maalum  wa Huruma, pamoja na Hati ya Kuangaza ya mwaka 2015, inazidi kuongezeka na leo hii kuna mapadre wapatao 1258 waliowekwa rasmi duniani kote katika huduma hiyo. Kwa Wamisionari, “ishara ya kujali kwa  Mama Kanisa Watu wa Mungu" (Misericordiae Vultus, n. 18), kitivo maalum kilitolewa kusamehe hata dhambi ambazo zimehifadhiwa kwa Kiti cha Kitume. Ratiba ya  Jubilei ya Wamisionari wa Huruma itaanza saa 4:00 asubuhi  siku ya Ijumaa tarehe 28 Machi, kwa sala katika Ukumbi wa Paulo VI itakayofungua Mkutano wa nne wa Dunia wa Wamisionari. Mkutano huo wa kimataifa unaoandaliwa na Baraza la Kipapa la  Uinjilishaji na kufanyika kila baada ya miaka miwili, utakuwa na mada kuu "Msamaha kama Chanzo cha Matumaini" na utagawanywa katika vipindi viwili vya mafunzo.

Dakika za kwanza asili ya kitaalimungu itatambulishwa saa 4.30 asubuhi na Askofu Mkuu  Rino Fisichella, Mwenyekiti Mwenza wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji, wakati katika kikao cha pili, kuanzia saa 6.00, kamili masaa ya Ulaya, huku saa 8 masaa ya Afrika Mashariki na Kati baadhi ya miongozo kwa ajili ya huduma yao ya kichungaji itapendekezwa kwa washiriki. Mkutano utaendelea saa 10:00 jioni kwa kuadhimisha toleo la XII la "Saa 24 kwa Bwana" katika Kanisa Kuu la Mtakatifu 'Andrea della Valle, lililotengwa kwa ajili ya Wamisionari. Mpango wa Kwaresima wa sala na upatanisho, ambao pia ulitamaniwa na Papa Francisko kwa mwaka 2013, utaadhimishwa pia katika majimbo yote ya duniani katika mkesha wa Dominika ya Nne ya Kwaresima, kati ya Ijumaa tarehe 28 na Jumamosi tarehe 29 Machi 2025. Kwa toleo hili, katika Mwaka wa Jubilei, Papa amechagua kauli mbiu muhimu sana: "Wewe ni tumaini langu" (Zab 71:5). Madhumuni ya tukio hilo ni kuweka sakramenti ya upatanisho kuwa kitovu cha maisha ya kichungaji ya Kanisa. Katika tovuti ya Baraza la Kipapa la Uinjilishaji, parokia na jumuiya za Kikristo zinaweza kupakua bila malipo nyenzo za kuadhimisha jumuiya ya liturujia.

Rozari, Misa na Tamasha

Siku ya Jumamosi tarehe 29 Machi 2025 Wamisionari watapata fursa ya kujionea, kati ya saa 3.00 na 5.00, Asubuhi hija yao kwenye Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Mtakatifu Petro. Kisha watakutana kusali Rozari katika Grotto ya Lourdes katika bustani ya Vatican. Tukio la Jubilei litahitimishwa Dominika tarehe 30 Machi 2025 kwa kuadhimisha Misa, itakayoongozwa na Askofu Mkuu Fisichella, kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Andrea della Valle saa 4:00 asubuhi, masaa ya Ulaya. Hatimaye, Dominika  alasiri, kwa Wamisionari na kwa yeyote anayetaka, kuwakuwa na  Tamasha la tano la Mwaka Mtakatifu lenye mada: "Jubilei ni Utamaduni" Mapitio yatafanyika: tamasha la bure.

Jubilei ya Wamisionari
26 Machi 2025, 16:24
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031