Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
PROGRAMU YA KISWAHILI
Ratiba Podcast
Askofu Mkuu  Bernardito Auza, Balozi wa Mpya Katika Umoja wa Ulaya (EU) Askofu Mkuu Bernardito Auza, Balozi wa Mpya Katika Umoja wa Ulaya (EU) 

Askofu Mkuu Auza ni Balozi mpya katika Umoja wa Ulaya

Papa Francisko amemteua Askofu mkuu mwenye makao ya Suacia kuwa na nafasi nyingine mpya.Tangu 2019 alikuwa anaongoza Ubalozi wa Vatican nchini Hispania na Andorra kwa kumpeleka katika Ofisi za Umoja wa Nchi za Ulaya(EU).

Vatican News

Jumamosi tarehe 22 Machi 2025 Baba Mtakatifu  alimteua Askofu Mkuu  Bernardito Cleopas Auza kuwa Balozi wa Vatican  katika Umoja wa Ulaya(EU). Mwenye umri wa miaka sitini na sita, ni mzaliwa wa Ufilipino, na ambaye amekuwa na utume wake katika huduma ya Vatican kwa muda mrefu. Mwaka 2008, alikuwa Balozi wa Vatican nchini Haiti, kisha mnamo mwaka  2014 alishika nafasi ya kuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican wa  Umoja wa Mataifa huko New York Marekani na vile vile kuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Shirika moja  la Marekani (OAS).

Baada ya miaka 5 ahadi yake bado alitumwa kuwa Balozi wa Vatican nchini Hispania na Andorra. Ana shahada ya Fasihi na Taalimungu. Anazungumza Kifaransa, Kiingereza, Kiitaliano, Kihispania na Kitagalogi. Nafasi hiyo ya katika Umoja wa Ulaya,  anamrithi Askofu Mkuu Noël Treanor, aliyefariki ghafla kwa mshtuko wa moyo mnamo tarehe 11 Agosti 2024. Katika ujumbe wa rambirambi, kuhusiana na marehemu huyo Papa Francisko  alitoa shukrani zake za kina kwa "huduma yake ya kujitolea na ya uaminifu" kwa ajili ya huduma ya Vatican.

Hongera kutoka kwa tume ya Comece

Baada ya kutangazwa kwa uteuzi wake, rais wa Tume ya Mabaraza ya Maaskofu ya Umoja wa nchi za Ulaya, (Comece) Askofu  Mariano Crociata alionesha furaha yake: "Askofu Mkuu Auza analeta urithi mashuhuri wa kujitolea kwa kidiplomasia na huduma ya kikanisa. Kwa miongo kadhaa alijikita na jukumu kuu katika huduma ya kidiplomasia ya Vatican akionesha kujitolea kwa kina na kuona mbele. Nina hakika kwamba ushirikiano wetu utakuwa na manufaa na matokeo katika kukuza manufaa ya pamoja katika Umoja wa Ulaya. Ninampatia matashi  yangu ya dhati kwa nguvu na hekima katika utume wake. Muongozo wa Mungu uwe pamoja naye katika kila hatua,” ndivyo tunasoma ujumbe wa Rais wa Tume ya COMECE.

Askofu Mkuu Auza Balozi wa Vatican katika UE
22 Machi 2025, 18:00
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031