Tafuta

Il Papa, 'ho fame di giustizia, si eliminino le cause della povert�' Tahariri

Neno la Papa daima ni lile la Mchungaji

Tafakari kuhusu nafasi ya Mfuasi wa Petro na kuhusu Majisterio yake.

Andrea Tornielli

Mrithi wa Petro hata anapozungumzia amani na vita, kuwakaribisha wahamiaji, au jinsi ya kubaki binadamu katika enzi ya akili unde, ni na bado ni kiongozi wa kiroho. Ikiwa ukweli kwamba Askofu wa Roma, kwa mujibu wa Mikataba ya Lateran ya 1929 iliyotatua "Suala la Roma," pia ni mkuu wa Taifa  dogo zaidi duniani— chini ya nusu kilomita ya mraba katikati ya mji mkuu wa Italia, haimaanishi kwamba anatenda au kujieleza kama mwanasiasa anapogusia masuala yanayohusu ubinadamu wetu.

Papa Paulo VI alielezea hili vizuri, akizungumza mnamo tarehe 4 Oktoba  1965, katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa: "Mkutano huu, ninyi nyote mnaelewa,” alisema Papa Montini, “unaashiria wakati rahisi na mzuri. Rahisi, kwa sababu ninyi mbele yenu mna mtu kama ninyi,  yeye ni kaka  yenu, na kati yenu, wawakilishi wa nchi huru,  mmoja wa zilizo ndogo zaidi, alijivika naye  ikiwa mnapenda kunifikiria hivyo, akiwa na uhuru mdogo, karibu wa kiishara wa muda, wa kutosha tu kwake kuwa huru kutekeleza utume wake wa kiroho, na kumhakikishia yeyote anayemshughulikia kwamba hana uhuru wa kila uhuru wa ulimwengu huu.” Papa, ambaye alikuwa amefika huko Marekani, mara moja aliongeza akizungumzia juu yake mwenyewe: "Yeye hana nguvu za muda, wala tamaa ya kushindana na ninyi, kiukweli hatuna la kuuliza, hakuna swali la kuuliza; japokuwa ni hamu ya kujieleza na ruhusa ya kuomba, ile ya kuweza kuwatumikia katika yale tunayopewa kufanya, bila maslahi,  kwa unyenyekevu na upendo."

Ni kweli, ili kuhakikisha uhuru kamili wa Kharifa wa  Kristo, karibu miaka mia moja iliyopita ilianzishwa kwamba kulikuwa na kiwanja kidogo cha ardhi ambapo Askofu wa Roma na Mchungaji wa Kanisa la Ulimwengu wote pia alikuwa huru, kwa hiyo mkuu wa Serikali.  Lakini ilikuwa na ni mkataba wa kutambua kwa usahihi hitaji hili la uhuru kutoka katika serikali nyingine yoyote na sio uthibitisho wa utume mara mbili. Kuinuliwa au kusisitiza kupita kiasi nafasi ya Papa kama mkuu wa nchi, msisitizo wowote juu ya umuhimu wa nafasi hii, kwa hivyo ni kupotosha kwa sababu kunadhoofisha dhamira yake moja ya kweli kama Mchungaji wa ulimwengu wote. Mchungaji anayezungumza na Wakatoliki, Wakristo, waamini, na watu wote wenye mapenzi mema kwa nia moja tu ya kutangaza Injili, ujumbe wake wa upendo, udugu, na amani "isiyo na silaha na ya kupokonya silaha".

Hili lilisisitizwa vyema na Kardinali Giovanni Battista Montini, aliyewahi kuwa Askofu Mkuu wa Milano, akizungumza katika Kilima cha Capitoline (Meya wa Mji)mnamo tarehe 10 Oktoba 1962, usiku wa kuamkia uzinduzi wa Mtaguso wa Pili la Kiekumeni wa Vatican. Katika hotuba hiyo, Papa wa baadaye, akizungumzia mwisho wa mamlaka ya kidunia ya Kanisa baada ya kuanguka kwa Sarikali ya  Upapa mnamo 1870, alisema: "Hapo ndipo upapa ulipoanza tena kwa nguvu isiyo na kifani nafasi yake kama mwalimu wa maisha na shuhuda wa Injili, ili kupanda hadi viwango vya juu katika utawala wa kiroho wa Kanisa na katika ushawishi wake wa kimaadili duniani kuliko hapo awali."

Anapoomba maisha ya mwanadamu yaheshimiwe na kulindwa kila wakati katika kila hatua ya uwepo wake, anapozungumzia amani, akifikiria mema ya watu na kutoa wito wa kukomeshwa kwa mbio za silaha za kichaa, hata kupita dhana ya "vita vya haki," anapotoa wito wa mazungumzo na majadiliano  akiita Majisterio ya Mafundisho Jamii, anapoomba kuwachukulia wahamiaji kama watu wa kukaribishwa bila kusahau hadhi yao ya kibinadamu, anapotukumbusha kwamba maskini ndiyo kitovu cha Injili na kwamba lazima tujenge jamii zenye haki na usawa zaidi, anapotetea haki ya uhuru wa kidini, anaposisitiza umuhimu wa kulinda kazi ya Uumbaji na kuupitisha kwa watoto na wajukuu zetu, Mrithi wa Petro haongei kama mkuu wa nchi. Anatangaza Injili tu.

NAFASI YA PAPA

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

13 Julai 2026, 17:22