Tafuta

2026.06.12 Ziara ya Kitume ya Papa Leo XIV-Mkutano na Wahamiaji katika Kituo cha Las Raíces, 2026.06.12 Ziara ya Kitume ya Papa Leo XIV-Mkutano na Wahamiaji katika Kituo cha Las Raíces,  (@Vatican Media) Tahariri

Wito kwa wafanyabiashara haramu wa binadamu na wajibu wetu

Maneno ya Papa Leo XIV kuhusu hali ya wahamiaji,akifuata nyayo za watangulizi wake

Andrea Tornielli

“Acheni! Tubuni!" Kilio cha Papa Leo XIV kutoka Uwanja wa Kristo huko Pawani ya Tenerife, kinakumbusha wito wa Mtakatifu Yohane Paulo II wa kuongoka kwa kikundi cha kihalifu cha mafia, uliotolewa mwishoni mwa Misa katika Bonde la Mahekalu huko Agrigento mnamo tarehe 9 Mei  1993.  Papa Wojtyła alikuwa akizungumza kuhusu wanachama wa Cosa Nostra na wakati; mrithi wake wa tatu alikuwa akilenga kuhusu wafanyabiashara haramu wa binadamu wanaowadanganya, kuwatumikisha, na kuwalazimisha wahamiaji kutafuta mustakabali wa kila aina ya vurugu. Papa Leo XIV, baada ya kusikiliza baadhi ya uzoefu wa wahamiaji, alisisitiza vifungu vyenye nguvu zaidi vya wito wake katika Maandiko: "Acheni! Tubuni!" yanarudia wito wa uongofu uliotamkwa na Yesu katika Injili ya Marko. Maneno, "Machozi na damu ya ndugu hawa yanamlilia Mungu, na mateso yao yanamfikia," yanakumbuka jinsi Mungu alivyoitikia mauaji ya Kaini kwa Abeli, kama tunavyosoma katika kitabu cha Mwanzo, na jinsi Mungu anavyosikiliza maumivu ya watu wake, kama tunavyosoma katika Kitabu cha Kutoka.

Mrithi wa Petro, ambaye katika siku mbili za mwisho za ziara  yake kwenda Hispania, akiwa na vituo huko Kisiwa Kikubwa cha Kanari  na Tenerife, alitaka kutimiza hamu iliyooneshwa na Papa Francisko ya safari, alionya: pesa zilizochukuliwa kutoka kwa ndugu hawa maskini hazitaleta amani, heshima, wala mustakabali wowote. Aliwaonya wafanyabiashara haramu ya binadamu, akimnukuu Mtakatifu Paulo katika Barua ya Pili kwa Wakorintho, kwamba,  kwa kila maisha yaliyopotea, kila familia iliyodanganywa, kila mwili unaotiishwa, kila mwanamke anayetishiwa, kila mfanyakazi anayenyonywa, "mnapaswa mjioneshe mbele ya haki ya Mungu."

Na aliwasihi wawaachilie huru wale waliofungwa utumwani, akikumbusha kwamba huruma  ya Mungu hutolewa hata kwa mwenye dhambi ngumu zaidi anayetumia udhaifu wa wanawake, watoto, wanaume, lakini "kupitia mlango mwembamba wa ukweli, haki, na uongofu," kama tunavyosoma katika Kitabu cha Nabii Ezekieli. Ingawa mvuto mkubwa na wa kinabii zaidi ni uongofu wa wafanyabiashara haramu wa binadamu, hatupaswi kusahau maneno mengine ambayo Papa Leo XIV  aliyasema wakati wa siku zake mbili katika Visiwa vya Kanari.

Hotuba ya Papa Leo  XIV kuhusiana ana hali halisi ya ufungamanishaji wa wahamiaji
Hotuba ya Papa Leo XIV kuhusiana ana hali halisi ya ufungamanishaji wa wahamiaji   (@Vatican Media)

Katika bandari ya Arguineguín, huko Las Palmas ya Kisiwa kikubwa cha Kanari,  Papa aliinama mbele ya hadhi ya wahamiaji, akikumbusha kwamba wao si "namba au faili" bali ni "watu wenye familia na nyumba waliyoiacha, wenye ndoto ambazo hakuna mtu mwenye haki ya kuzidharau." Na alisema wazi kwamba maisha yao "lazima yalindwe." Kisha Papa Leo XIV alitaka uchunguzi wa dhamiri "kwa mataifa ya asili, ambayo lazima yatengeneze mazingira ya amani, haki, na maendeleo; kwa mataifa ya usafiri, yaliyoitwa kulinda na kutowaacha wanyonge kwenye mitandao ya uhalifu; kwa Ulaya, ambayo haiwezi kutangaza utu wa binadamu na kuzoea Mediterania na Atlantiki kuwa makaburi bila mawe ya makaburi; kwa Jumuiya ya kimataifa, iliyoitwa kwa ushirikiano mzuri na endelevu."

Pia alihutubia Kanisa, ambalo "lazima lijiruhusu kupingwa" kwa sababu "mapokezi ya wahamiaji hayawezi kuwa kitu cha pili, wala kukabidhiwa kwa watu wachache tu wa kujitolea," na hatuwezi kupiga magoti mbele ya madhabahu kumwabudu Kristo katika Ekaristi na kisha kupita mbele ya mateso ya ndugu zetu hawa. Katika bandari ya Arguineguín, Askofu wa Roma, akitoa wito wa "njia salama na halali, misaada na usaidizi, ushirikiano wa kweli dhidi ya wafanyabiashara haramu, ulinzi mzuri wa waathiriwa, michakato mikubwa ya kuwakaribisha na kuwaunganisha, na sera zinazomruhusu kila mtu kuishi kwa heshima katika nchi yake," pia aliwaalika kila mtu, mabunge ya kiraia, serikali, mashirika ya kimataifa, na hata jumuiya za Kikristo, kuuliza swali la kina, ambalo linaweza kuelezewa kama "kimuundo:" Je "Tumejenga ulimwengu wa aina gani ikiwa kaka na dada wengi wanapaswa kuhatarisha kifo wakitafuta maisha?"

Ziara ya Visiwa vya Kanari inaashiria hatua muhimu katika upapa wake. Kama Papa Francisko alivyofanya huko Lesbos, Papa Leo XIV pia alichagua kukumbuka familia ya Nazareti mtoto Yesu, Maria na Yosefu ambao walilazimika kukimbilia Misri ili kuokoa maisha ya Mwana wa Mungu, ambaye ghadhabu ya Herode iliangukia dhidi yake. Familia hiyo, Familia Takatifu, "inabaki kuwa kielelezo na kimbilio la milele kwa kila familia ya wakimbizi, kwa kila mhamiaji, na kwa kila mtu aliyelazimishwa kuondoka katika nchi yake kwa sababu ya hofu, mateso, au ulazima," Papa alikumbuka, akinukuu Katiba ya Kitume ya Pio  XII "Exul Familia." Wakristo hawawezi kusahau kwamba Mwanadamu wao aliyeumbwa na Mungu alikuwa mhamiaji na mkimbizi. Kwa sababu hii, wanaitwa kutambua uso wake katika nyuso za dada na kaka wanaogonga milango ya nchi zetu wakitafuta mustakabali.

Wito mkali wa Papa kwa wanaotumia unyonge wa binadamu kwa faiza zao
Wito mkali wa Papa kwa wanaotumia unyonge wa binadamu kwa faiza zao   (@Vatican Media)
TAARIRI KUHUSU HOTUBA YA PAPA HUKO KANARI

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here

12 Juni 2026, 12:58