Papa anaelekea Las Palmas de Gran Canaria
Vatican News
Baba Mtakatifu Leo XIV aliondoka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Josep Tarradellas Barcelona-El Prat kuelekea Las Palmas de Gran Canaria saa 2.45, Alhamisi asubuhi tarehe 11 Juni 2026. Hii inakuwa kituo cha tatu cha Ziara yake ya kitume, mara baada ya kuadhimisha misa katika Basilika ya Familia Takatifu huko Barcelona usiku wa tarehe 10 Juni 2026 na kuzindua mnara wa Kanisa Kuu hilo.
Kwa ziara hii ya visiwa vikubwa katika Bahari ya Atlantiki, ambavyo pia zitajumuisha kituo kingine cha Santa Cruz de Tenerife, Papa Leo XIV atahitimisha Ziara yake ya nne ya kitume nchini Hispania iliyoanza tangu tarehe 6 Juni.
Kwaheri kutoka Barcelona
Alhamisi takriban saa 7:30 asubuhi, Papa Leo XIV aliondoka nyumbani kwa Askofu Mkuu kuelekea uwanja wa ndege, ambapo alipokelewa na mamlaka mahalia. Kisha Papa Leo XIV alipanda ndege ya Iberia A320, ambayo, ndani ya saa tatu na nusu, itampeleka kwenye kituo cha anga cha Gran Canaria-Gando. Kwa mujibu wa utamaduni, mamlaka mahalia zitakuwepo kumkaribisha, ikifuatiwa na mkutano katika ukumbi wa watu mashuhuri.
Mkutano na Vituo vya mapokezi vya wahamiaji
Kituo cha kwanza katika ziara ya Papa katika Visiwa vya Kanari kitakuwa mkutano na vituo vya mapokezi vya wahamiaji katika bandari ya Arguineguín, kwenye pwani ya kusini ya kisiwa cha Kanari. Bandari hii bado inajulikana kama "Bandari ya Aibu" kwa sababu mnamo 2020, muda mfupi baada ya kuzuka kwa dharura ya Uviko19, takriban wahamiaji 3,000 walifika huko ndani ya Juma moja. Hata hivyo, kutokana na janga hilo, hakuna mtu aliyeruhusiwa kuingia bandarini: ni Caritas pekee iliyopanga shughuli zake kusaidia ajali ya meli iliyoharibika, ikileta chakula na vifaa vya matibabu. Mtu wa kujitolea kutoka shirika hilo atakuwa miongoni mwa wale watakaoshiriki ushuhuda wao na Papa.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here
