Tafuta

2026.06.08 Mkutano wa Faraka na Bwana Pedro Sanchez Perez-Castejo,Waziri Mkuu wa Hispania. 2026.06.08 Mkutano wa Faraka na Bwana Pedro Sanchez Perez-Castejo,Waziri Mkuu wa Hispania.  (@Vatican Media)

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Hispania,Sánchez

Ulikuwa mkutano mfupi wa faragha wa asubuhi Jumatatu tarehe 8 Juni 2026 kabla ya kuelekea kwenye mkutano wake katika Bunge la Hispania.

Vatican News

Kabla ya kufika katika Bunge la Manaibu kwa ajili ya mkutano na wabunge wa Bunge la Hispania asubuhi ya Jumatatu tarehe 8 Juni 2026 ikiwa ni siku yake ya tatu  katika Ziara yake ya Kitume nchini Hispania, akiwa Madrid, Papa Leo XIV alikutana kwa muda mfupi na Waziri Mkuu, Pedro Sánchez Pérez-Castejón.

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Hispania kwa faragha
Papa akutana na Waziri Mkuu wa Hispania kwa faragha   (@Vatican Media)

Ofisi ya Habari ya Kiti Kitakatifu iliripoti hili kwenye chaneli yake ya Telegram, ikibainisha kwamba Papa baadaye aliwasalimia baadhi ya washirika wake. Mkutano huo wa faragha ulidumu kwa takriban dakika 20.

Papa amekutana na Waziri Mkuu kwa faragaha
Papa amekutana na Waziri Mkuu kwa faragaha   (@Vatican Media)


Mara ya Mwisho alikuwa amekutana naye hivi karibuni mnamo tarehe 27 Mei 2025 mjini Vatican.

Papa na Waziri Mkuu wa Hispania

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

08 Juni 2026, 10:48