Tafuta

2026.06.09 Papa akutana na Washiriki wa Mkutano wa Mediterranea(MED26). 2026.06.09 Papa akutana na Washiriki wa Mkutano wa Mediterranea(MED26).  (@Vatican Media)

Barcelona,Papa akutana na wawakilishi wa MED26:changamoto nyingi katika Mediterrania

Papa Leo XIV alifanya mazungumzo alasiri katika jiji la Kikatalani,kuanzia majadiliano ya kitaasisi hadi yale yaliyofanywa na maaskofu,vijana,na wafanyakazi mbalimbali wa kijamii wanaoshiriki katika Mkutano wa Mediterania wa MED26,unaofanyika Barcelona hadi Juni 12.Aliwasihi wafanye dunia kuwa mahali pazuri zaidi.

Vatican News

Papa alikuwa na mikutano kadhaa alasiri ya Jumanne tarehe 9 Juni 2026 hasa mara baada ya kufika katika Ukumbi wa Askofu Mkuu wa Barcelona. Kwa mujibu wa Ofisi ya Habari ya Vatican iliripoti hilo kupitia Telegram. Ulifanyika Mkutano na Mkuu wa Mkoa wa Katalonya, Salvador Illa i Roca, ambao ulidumu kwa takriban dakika 15. Mwishoni, Papa Leo XIV pia aliwasalimu baadhi ya washirika wake.

Papa akutana na Jenerali wa Katalonya
Papa akutana na Jenerali wa Katalonya   (@Vatican Media)
Mkuu wa Mkoa wa Katalonya na Papa
Mkuu wa Mkoa wa Katalonya na Papa   (@Vatican Media)

Kuelekea bandari ambapo habari njema inasubiriwa
Takriban washiriki 200 wanahudhuria Mkutano wa Mediterania wa MED26, ambao kwa sasa unafanyika huko Barcelona, sambamba na Ziara ya Papa ya Hispania, na ambao Papa Leo XIV alikutana nao. Aliwahutubia, huku akiwatia moyo kusafiri, kijiografia na kiroho, hadi bandari hizo ambapo wanaume na wanawake wanasubiri habari njema. Kisha alitaja changamoto nyingi zinazokabili Mediterania, hasa Mashariki ya Kati, na kutoa shukrani na kutia moyo kwa kazi inayolenga kuifanya dunia kuwa mahali pazuri, katika kujenga mazungumzo, na kuona kwamba "kuna utajiri katika utofauti, na katika utofauti tunaweza kuungana." Mwishoni mwa mkutano, walisali pamoja na sala ya Baba Yetu.

Papa alikutana na MED26
Papa alikutana na MED26   (@Vatican Media)

Mkutano wa MED26 unaoongozwa na mada kwa ajili ya "ujenzi wa amani" katika Bahari ya Mediterania. Mnamo Machi 12, Papa Leo XIV ilikuwa amepokea ujumbe kutoka Ofisi ya Uratibu wa Kanisa la Mediterania, inayoongozwa na Kardinali Jean-Marc Aveline, huko Vatican akiwatia moyo waliohudhuria kuendelea na mipango yao ya kukuza elimu ya amani na utamaduni wa kukutana.

Papa akiwajongea wa MED26
Papa akiwajongea wa MED26   (@Vatican Media)
PAPA AKUTANA NA MED26

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here

 

09 Juni 2026, 20:05