Wasiwasi wa Papa Leo kuhusu mashambulizi ya kigaidi katika maeneo ya Sahel
Na Angella Rwezaula – Vatican.
“Nawahakikishia maombi yangu kwa ajili ya waathiriwa na ukaribu wangu na wote wanaoteseka. Ninatumaini aina zote za vurugu zitaisha na kuhimiza kila juhudi kwa ajili ya amani na maendeleo katika nchi hiyo pendwa." Haya ni maneno ya wasi wasi na kutia moyo ya Baba Mtakatifu Leo XIV, aliounesha mara baada ya sala ya Malkia wa Mbungu, akiwa katika dirisha la Jumba la Kitume, kwa kuwageukia waamini na mahujaji waliotoka pande za dunia wakiwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican, Dominika tarehe 10 Mei 2026.
Papa Leo XIV akianza alisema: “Kaka na dada wapendwa, nimepokea kwa wasiwasi kuhusu habari za ongezeko la vurugu katika eneo la Sahel, hasa Chad na Mali, zilizokumbwa na mashambulizi ya kigaidi ya hivi karibuni. Papa Leo XIV aliendelea: “Nawahakikishia maombi yangu kwa ajili ya waathiriwa na ukaribu wangu na wote wanaoteseka.Ninatumaini aina zote za vurugu zitaisha na kuhimiza kila juhudi kwa ajili ya amani na maendeleo katika nchi hiyo pendwa.”
Siku ya Kirafiki kati ya Kanisa la Kikopti na Kikatoliki
Kila mwaka, ifikapo Mei 10 huadhimishwa "Siku ya Urafiki wa Wakopti na Wakatoliki." Baba Mtakatifu Leo XIV aliongeza: “Ninatoa salamu za kidugu kwa Patriaki Tawadros II na kuwahakikishia Kanisalote pendwa la Wakopti maombi yangu, na kwa matumaini kwamba safari yetu ya urafiki itatuongoza kwenye umoja kamili katika Kristo, aliyetuita ‘marafiki.’”(Yh 15,15).
Kisha Papa alitoa salamu zake kwa wote kuanzia na warumi, na mahujaji kutoka Nchi mbalimbali. Kwa nama ya pekee aliwasalimu Kikundi cha “Walinzi wa Heshima cha Moyo Mtakatifu wa Yesu,” kutoka sehemu mbali mbali za Italia. Watu wa “kujitolea kwa ajili ya Uinjilishaji,” kinachohusiana na Familia ya Radio Maria; Chama cha Kujitolea cha “Komen Italia”, ambacho kinajikita na kuhamasisha kuzuia sarani za matiti.
Papa kwa lugha ya kispanyola alisema: “Ninapanda kutoa shukrani zangu kwa ukaribisho wa joto unaowatambulisha watu wa Visiwa vya Canari, na kuruhusu meli ya kitalii ya Hondius kutia nanga na wagonjwa wa hantavirus. Ninafurahi kuweza kukutana nanyi mwezi ujao wakati wa ziara yangu kwenye visiwa hivyo.”
Siku ya Mama
Papa Leo XIV katika muktadha wa siku ya Mama alisema: “Wazo pia maalum linawageukia Mama wote. Kwa maombezi ya Maria, Mama wa Yesu na wetu, tuombe kwa upendo na shkrani kwa kila mama, hasa kwa wale wanaoishi katika hali ngumu zaidi. Asante. Mungu awabariki!
Hatimaye Papa aliwatakia Dominika njema na kuwaaga.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.
