Tafuta

Kumbukizi ya miaka 40 ya ajali mbaya ya  nuvu za kinyuklia za Chernobyl kunako 1986. Kumbukizi ya miaka 40 ya ajali mbaya ya nuvu za kinyuklia za Chernobyl kunako 1986.  (AFP or licensors)

Papa Leo XIV,waathiriwa wa Nyuklia ya Chernobyl:Nguvu ya atomiki iwe ya amani

Katika kumbukizi ya miaka 40 ya ajali kubwa ya nyuklia ya Chernobyl iliyotokea katika kiwanda cha nguvu za nyuklia,Papa aliwakumbuka waathirika wa janga baya zaidi katika historia na kuwakumbusha jumuiya ya Kimataifa kuhusu hatari za nguvu za nyuklia."Katika ngazi zote,acheni utambuzi na uwajibikaji vitawale."

Na Angela Rwezaula – Vatican

Baba Mtakatifu Leo XIV, mara baada ya sala ya Malkia wa Mbingu akiwa katika Dirisha la Jumba la Kitume, Dominika tarehe 26 Aprili 2026 alikumbuka ajali mbaya iliyotokea huko Chernobyl nchini Ukraine ambayo "iliathiri dhamiri ya binadamu" na kusema: "Leo inaadhimishwa miaka 40 ya ajali mbaya ya Chernobyl, ambayo iliathiri dhamiri ya binadamu. Inabaki kuwa onyo la hatari zinazotokana na matumizi ya teknolojia zenye nguvu zaidi.”

Papa Leo XIV aliongeza: “Tunawakabidhi waathiriwa na wote ambao bado wanakabiliwa na matokeo hayo kwa huruma za Mungu. Kwa kugeukia ngazi za kimataifa, Papa aliongeza kusema: "Ninatumaini kwamba, katika ngazi zote za kufanya maamuzi, utambuzi na uwajibikaji vitashinda kila wakati, ili kila matumizi ya nishati ya atomiki yawe katika huduma ya maisha na amani.”

Salamu kwa mahujaji

Kisha Papa aliwageukia mahujaji na waamini kuanzia na Warumi na mahujaji kutoka nchi mbalimbali: na kuwakaribisha. Nawasalimu Shirika Kijeshi  kike na kiume la Mtakatifu George, Shirika la Ulaya la Nyumba ya Habsburg-Lorraine. Nawasalimu watoto wa kikundi cha densi cha "Malva" kutoka Brovary, Ukraine; Kwaya ya ‘Cantica Sacra ya Jimbo Kuu la Trnava, Slovakia; waamini kutoka Vienna, Madrid, na Visiwa vya Canari;

Kadhalika Papa Pia aliwapa salamu Wakurugenzi na Walimu wa Shule ya "São Tomás" huko Lisbon. Nawasalimu kundi kubwa la watoto kutoka Val Camonica (Jimbo la Brescia) na wahudumu wa Altreni kutoka Biadene na Caonada; pamoja na waamini kutoka Treviso, Vicenza, Crotone na Cariati, Oria, na Lecce; na washiriki katika mkutano wa Chama cha Mitume wa Huruma ya Mungu.

Salamu kwa wazazi na marafiki wa Mapadre wapya wa Roma

Salamu maalum kwa familia na marafiki wa mapadre wapya wa Jimbo Kuu la Roma, ambao Papa aliwaweka wakfu Asubuhi ya Dominika Aprili 16 katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro ambapo Papa ameimba kwamba "daima wasindikizwe, hawa wahudumu vijana wa Injili kwa maombi." Alihitimisha kuwatakia Dominika Njema

Kuhusiana na ajali hii mbaya ya Chernobly

Ilikuwa yapata Saa 7:23 za usiku wa kuamkia tarehe 26 Aprili  1986, ambapo hitilafu katika mtambo wa nyuklia nambari 4 katika kiwanda cha nguvu za nyuklia cha Chernobyl ilittokea na kulipuka, karibu na Kyiev, mji wa Ukraine, na kusababisha ajali mbaya zaidi ya nyuklia katika historia ya nguvu za nyuklia. Mlipuko huo uliharibu sehemu ya ndani ya jengo, ukitoa wingu la moshi wenye mionzi angani. Kabla ya kuenea Ulaya yote, ulichafua maeneo makubwa ya Ukraine, Belarusi, na Urusi, na kulazimisha maelfu ya watu kuhama. Kuna watu ambao hawakurudi majumbani mwao, wakiacha kabisa eneo kubwa ambalo bado linachukuliwa kuwa "lisiloweza kukaliwa." Kwa hiyo ni baada ya miaka 40 ya  kumbukumbu ya maafa mabaya zaidi ya nyuklia katika historia, ambayo yalisababisha uharibifu usiohesabika kwa afya ya binadamu na kasoro kubwa za kijenetiki kwa watoto ambao hawajazaliwa.

Papa baada ya miaka 40 ya ajali ya Chernobyl

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

26 Aprili 2026, 12:31

Sala ya Malkia wa Mbingu ni nini?
 

Utenzi wa Malkia wa Mbingu ni kati ya tenzi nne za Bikira Maria (nyingine ni:Tunakimbilia Ulinzi wako,  Salam Malkia wa Mbingu, Salam Malkia). Kunako mwaka 1742, Papa Benedikto XIV alipoandika kwamba, waamini wasali Sala ya Malkia wa Mbingu wakiwa wamesimama, kama alama ya ushindi dhidi ya kifo, wakati wa Kipindi cha Pasaka, yaani kuanzia Domenika ya Ufufuko wa Bwana hadi Sherehe ya Pentekoste. Hii ni Sala ambayo husaliwa mara tatu kwa siku kama ilivyo pia Sala ya Malaika wa Bwana: Asubuhi, Mchana na Jioni ili kuweka wakfu Siku kwa Mwenyezi Mungu na Bikira Maria.

Utenzi huu kadiri ya Mapokeo ulianza kutumika kunako karne ya VI au Karne X, lakini kuenea kwake kunaanza kujitokeza katika nyaraka mbali mbali kati kati ya Karne ya XIII, ilipoingizwa kwenye Kitabu cha Sala za Kanisa cha Wafranciskani. Hii ni Sala inayoundwa na maneno mafupi manne yanayohitimishwa na Alleluiya na sala ya waamini wanaomwelekea Bikira Maria, Malkia wa mbingu, ili kufurahia pamoja naye kuhusu Fumbo la Ufufuko wa Kristo Yesu.

Papa Francisko tarehe 6 Aprili 2015 wakati wa Sala ya Malkia wa Mbingu, siku moja baada ya Sherehe ya Pasaka, aliwashauri waamini kuwa na moyo wa furaha wanaposali sala hii. “Tunamwendea Bikira Maria, tukimwomba afurahi, kwa sababu yule Mwanaye mpendwa aliyekuwa amemchukua mimba amefufuka kweli kweli kama alivyosema; tunajiaminisha kwa sala na maombezi ya Bikira Maria. Kimsingi furaha yetu ni mwangi wa furaha ya Bikira Maria kwani ndiye aliyetunza na anaendelea kutunza matukio mbali mbali ya maisha ya Yesu. “Tusali sala hii kwa furaha ya kuwa waana wa Mungu ambao wanafurahi kwa sababu Mama yao anafurahi”

 

Sala ya Malaika wa Bwana/ Malkia wa Mbingu ya hivi karibuni

Soma yote >