Tafuta

Mambo muhimu katika siku ya sita ya Papa Leo XIV barani Afrika

Siku ya mwisho kati ya siku tatu alizotumia Papa nchini Cameroon ambapo aliongoza Misa katika uwanja wa ndege wa Yaoundé-Ville,kabla ya kuondoka kwenda mji mkuu wa Angola,Luanda,ambapo alikutana na Rais wa Jamhuri,mamlaka na Maaskofu wa nchi hiyo.

Vatican News

Jumamosi asubuhi tarehe 18 Aprili 2026, Pap Leo XIV aliongoza Ibada ya Misa Takatifu katika Uwanja wa Ndege wa Yaoundé-Ville, katika siku yake ya  mwisho kati ya tatu alizotumia nchini Cameroon, na kwa  siku yake ya  sita ya Ziara yake ya kitume barani Afrika.

Kuagana na mwenyeji wake Cameroon
Kuagana na mwenyeji wake Cameroon   (@Vatican Media)

Baada ya kufika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Yaoundé-Nsimalen, aliaga mamlaka ya kiraia na kidini ya nchi hiyo na saa 6:47 mchana saa za huko aliondoka kuelekea Luanda, mji mkuu wa Angola, ambapo alitua katika Uwanja wa Ndege wa "4 de Fevereiro" yapata saa 8:45 mchana saa za huko(ikiwa ni saa 9:45 alasiri saa za Roma).

Papa aliwasili
Papa aliwasili   (@Vatican Media)

Katika Uwanja wa Ndege alipokelewa na Rais wa Jamhuri hiyo Bwana João Manuel Gonçalves Lourenço, na vile vile katika Ikulu ya Rais na kukutana na mamlaka, asasi za kiraia, na kikundi cha kidiplomasia cha nchi hiyo.

Papa akipokea maua kutoka kwa watoto wawili wadogo wa kike
Papa akipokea maua kutoka kwa watoto wawili wadogo wa kike   (@Vatican Media)
Ziara ya faragha kwa Rais
Ziara ya faragha kwa Rais   (@Vatican Media)
Nje ya Ubalozi wa Vatican nchini Angola
Nje ya Ubalozi wa Vatican nchini Angola   (@Vatican Media)
Ndani ya Ua wa Ubalozi wa Vatican nchini Angola
Ndani ya Ua wa Ubalozi wa Vatican nchini Angola   (@Vatican Media)

Yapata saa 1:00 usiku kwa saa za huko, Papa alifanya pia mkutano wa faragha na Maaskofu Katoliki wa Angola.

Papa Juu ya Ubalozi wa Vatican nchini Angola
Papa Juu ya Ubalozi wa Vatican nchini Angola   (@Vatican Media)

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here

18 Aprili 2026, 19:43