Tafuta

2026.04.27 Papa Leo XIV alikutana na Kardinali Ernest Simoni(97) wa Albania. 2026.04.27 Papa Leo XIV alikutana na Kardinali Ernest Simoni(97) wa Albania.  (@Vatican Media)

Kardinali Simoni akutana na Papa Leo XIV:Nilimpatia masalia ya mashahidi wa Albania

Kardinali huyo wa Albania mwenye umri wa miaka 97 alizungumza na vyombo vya habari vya Vatican kuhusu mkutano wa asubuhi Jumatatu tarehe 27 Aprili na Papa Leo XIV mjini Vatican,pamoja na baadhi ya wanafamilia wake:"Tutangazie pamoja kwa watu wote wa dunia amani itokayo Mbinguni."

Pd.Davide Djudjaj – Vatican.

"Furaha yote, matumaini yote." Hivi ndivyo Kadinali Ernest Simoni, mwenye umri wa miaka 97, wa Albania, alivyosema hata baada ya kuteswa nchini mwake wakati wa utawala wa kikomunisti, akizungumza na mwandishi wa habari wa Vatican News, kuhusu mkutano wake na Papa Leo XIV, mnamo tarehe 27 Aprili 2026. Mbali na Kadinali huyo, alikuwa amezungukwa karibu wanafamilia wake arobaini, waliomsindikiza katika Ukumbi wa Mapapa mjini Vatican. "Ilikuwa mazingira ya furaha yote, matumaini yote, kutazama uso wa Baba Mtakatifu, ambao unawakilisha uso wa Yesu, kuwatangazia watu wote habari za Mbinguni, za amani, za udugu, na za upendo kwa watu wote wa dunia," Kardinali Simoni alibainisha.

Papa alikutana na Kardinali Ernest Simoni
Papa alikutana na Kardinali Ernest Simoni   (@Vatican Media)

"Shahidi Aliye Hai"

Tayari kunako tarehe 5 Aprili  iliyopita, ya Dominika ya  Pasaka, Kardinali wa Albania alikuwa pamoja na Kadinali Protodeacon Dominique Mamberti, pamoja na Papa Leo XIV wakati wa ujumbe na baraka ya Urbi et Orbi kutokea kwenye Dirisha la katikati ya Basilika ya  Mtakatifu Petro, mjini Vatican. Kardinali wa  Jimbo Kuu la Shkodra-Pult (Scutari), aliyesherehekea miaka 70 ya kuwekwa wakfu kwake mnamo Aprili 7, aliteswa nchini Albania. Alipokamatwa wakati wa Noeli 1963, alihukumiwa kwanza kifo na kisha kufanya kazi ya kulazimishwa katika mifereji ya maji taka ya Shkodra, na baadaye akatekeleza huduma yake kwa siri hadi kuanguka kwa utawala wa kikomunisti.

Mkutano wa Papa na Kardinali Simoni
Mkutano wa Papa na Kardinali Simoni   (@Vatican Media)

Papa Francisko alikuwa amesikiliza ushuhuda wake wakati wa Ziara yake ya Kitume  yake kwenda Albania mnamo Septemba 2014, akionekana kuguswa na kutokwa machozi na maneno ya Padre huyo, ambaye alimwita "shahidi aliye hai." Na mnamo 2016, Papa Francisko alimuumba kuwa Kardinali, kwa heshima huku akimshukuru kwa ushuhuda huu "ambao ni mzuri kwa Kanisa."

Kukutana na Papa ni neema maalum

Kwa hivyo, Mkutano huo na  Papa Leo VIX: "Hakika ilikuwa neema maalum niliyopewa na Roho Mtakatifu," alisema Kardinali Simoni, "na pia na Baba Mtakatifu, kutangaza pamoja, kwa watu wote wa ulimwengu, amani itokayo Mbinguni, amani tamu zaidi, furaha ya kiroho, na furaha ya ufufuko. Na kila kitu kiko hapa: imani, pamoja na ufufuko, itakuwa na furaha ya milele ambayo Yesu aliandaa kwa kumwaga damu yake yote kwa watu wote wa ulimwengu na wa rika zote."

Papa alimzawadia Papa Masalia ya Mashahidi wa Albania
Papa alimzawadia Papa Masalia ya Mashahidi wa Albania   (@Vatican Media)

Kardinali, ambaye, licha ya umri wake, aliishi Firenze kwa miaka kadhaa na anaendelea kusafiri ulimwenguni, alimpatia  Papa zawadi maalum mwishoni mwa kutano na kusema kwamba: "Nikija Italia kutoka Albania, mawazo yangu yako pamoja na mashahidi," na hivyo Kardinali Simoni aliwasilisha "msalaba na masalia ya mashahidi wa Albania waliotoa maisha yao kwa ajili ya uaminifu, kwa ajili ya upendo wa Yesu, kwa ajili ya wokovu wa watu wa Albania, ili kuwaona watu wote wakitabasamu Mbinguni."

Kardinali Simini aliambatana na wanafamilia wake
Kardinali Simini aliambatana na wanafamilia wake   (@Vatican Media)

Imesasishwa tarehe 28 Aprili 2026, saa 4.59 asubuhi na Angella Rwezaula.

KARDINALI SIMONI AKUTANA NA PAPA LEO XIV

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here

28 Aprili 2026, 10:36