Tafuta

2026.04.18 Mtoto akimkaribisha Papa kwa maua mara baada ya kufika Angola. 2026.04.18 Mtoto akimkaribisha Papa kwa maua mara baada ya kufika Angola.  (@Vatican Media) Tahariri

Hija ya Papa barani Afrika:wito wa kubadili mioyo

Katika hija ya Papa Leo XIV katika mataifa ya Afrika inaonesha nguvu ya watu,waliokandamizwa na nira ya kikoloni na anatuomba tuwe sehemu ya wakati uliopo na ujao wenye haki zaidi,udugu na mshikamano.

Massimiliano Menichetti

Ziara ya Kitume  ya Papa Leo XIV barani Afrika inatuomba tufungue macho yetu, tubadilishe mapigo ya mioyo yetu ili kuifanya iwe hai zaidi, na tutende ili uso wa ubinadamu uwe wa kweli zaidi. Katika siku hizi, maelfu ya watu wanamsubiri na kumsindikiza Baba Mtakatifu, wakijazana katika barabara nyekundu za udongo au mitaa ya jiji; na mara wakiwa nyingi nyuma ya kamba, ambapo kuna nyumba zenye paa za bati, majengo yaliyochakaa, au yanayobomoka, lakini macho ya kila mtu yamejaa furaha, na tabasamu hutoka mara tu mtu anapokutanisha na salamu. Watu wanasubiri kwa saa nyingi gari la Papa au msafara wake upite, unaoambatana nao ili nao wapate fursa ya kushiriki hata picha, kumbukumbu, wanaimba, wanacheza, wanapunga bendera na matawi, na wanainua mikono yao juu kwa nguvu. Ziara hii ni safari ya kuelekea kwenye majeraha na matumaini ya watu ambao mara nyingi husahaulika, lakini pia ni mwaliko kwa kila mtu kubadilisha mtazamo wao, wasigeuke, kujenga vifungo, udugu, na mahusiano bila kujisalimisha kwa hofu na kujiuzulu.

Afrika ambayo Papa Leo  anakabiliana nayo inaonesha uhai na nguvu nyingi, uwezo usio na kikomo kwa siku zijazo, lakini dhahiri pia ni nira ya kikoloni ambayo ulimwengu unaendelea kutumia ili kuponda, kudhibiti, na kukandamiza uwezo. Hapa, ambapo rasilimali zinaporwa, dunia inaharibiwa na taka zenye sumu, migogoro, upinzani, na ufisadi huchochewa, kinacholiwa na makundi yenye nguvu ya kisiasa na kiuchumi si pesa bali ni sasa na mustakabali wa vizazi vizima. Katika sayari iliyojeruhiwa na vita na vurugu, Mrithi wa Petro badala yake hujenga madaraja, kuhamaisha makutano, maridhiano, ufahamu, umoja, na amani. Hivi ndivyo ilivyokuwa huko Bamenda, ambayo wakati wa ziara yake iliunganishwa tena na nchi. Kutokana na vurugu zinazohusiana na suala la kujitenga, ambalo limesababisha maelfu ya watu waliokimbia makazi yao na vifo, barabara ziliharibiwa karibu kabisa, na uwanja wa ndege ulikuwa hautumiki kwa miaka minane. Kuwasili kwa Papa  Leo kumeamsha sio tu maendeleo ya kimwili, bali pia moyo, na kuamsha tena matumaini yaliyotulia.

Kwa ziara  zake, Papa pia anaakisi tofauti za mataifa anayoyatembelea na kuondoa simulizi la kutatanisha na la muhimu ambalo mara nyingi huiona Afrika kana kwamba ni nchi moja na si bara. Anaonesha kwa nguvu umoja katikati ya tofauti, upekee wa familia ya kibinadamu ambayo kila mtu ni sehemu yake kama mtoto wa Mungu. Anaonesha ulinganifu wa Kanisa, lililoitwa kueneza uzuri wa Injili, ambayo, ikifanyika mwili, huchochea ubunifu na kujenga jamii zenye haki zaidi, udugu, na usaidizi. Papa anatoa wito wa uwajibikaji wa pamoja, na kutoka Afrika anazungumza na ulimwengu, na kila mmoja wetu. Anauliza swali gumu linalotusukuma kuwafikia wengine, kukutana nao, kuwasamehe, kuwasaidia, kutembea pamoja, kuchukua jukumu la kujenga upeo mpya wa pamoja. Katika ulimwengu ambao mara nyingi huchochewa na mgawanyiko, kiburi, na vitisho, Baba Mtakatifu ana uso wa Kristo, ambaye anawaomba kila mtu kubadilika, akionesha "ndiyo" ya uongofu katika kila tendo la maisha ya kila siku. Papa Leo anaunganisha tena ubinadamu wote, akiwarudishia watu heshima na uhuru wa kukua na kustawi, akivunja madai ya kutawala na kumiliki.

Papa alishrirki Rozari hadi usiku na waamini huko Muxima
Papa alishrirki Rozari hadi usiku na waamini huko Muxima   (@Vatican Media)

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.

20 Aprili 2026, 09:12