Tafuta

2025.11.11 Chiesa di Sant'Anselmo all'Aventino - Santa Messa nel 125° anniversario della Dedicazione della Chiesa

Ujumbe wa Papa wa Siku ya Miito duniani 2026:'Ugunduzi wa Ndani wa Zawadi ya Mungu'

Katika Ujumbe wa Papa Leo XIV wa Siku ya kuombea Miito Ulimwenguni itakayoadhimishwa Aprili 26 anabainisha:"Kila wito ni zawadi isiyopimika kwa Kanisa na kwa wale wanaoipokea kwa furaha.Mtazamo wa Bwana wa upendo huangaza mioyo.Mtakatifu Yosefu aliamini hata wakati wote ulionekana kufunikwa na kutokuwa na uhakika na hivyo tupaswa kuwa na Yesu katika kila hali ya maisha huku tukimwilishwa na uhusiano wa kila siku naye."

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV katika Siku ambayo Mama Kanisa anaadhimisha Sherehe ya Kupashwa kwa Bikira Maria Habari jema, ametoa ujumbe wake kwa ajili ya Siku ya 63 ya Kuombea Miito Ulimwenguni, ambayo itaadhimishwa tarehe 26 Aprili 2026, ikiwa ni Dominika ya Nne ya Pasaka ijulkanayo Dominika ya Mchungaji Mwema. Katika Ujumbe huo unaongozwa na Kauli mbiu "Ugunduzi wa ndani wa Zawadi ya Mungu” anaiita siku hiyo kama neema ambapo tunashiriki tafakari kadhaa kuhusu mwelekeo wa ndani wa wito, unaoeleweka kama ugunduzi wa zawadi ya bure ya Mungu inayochanua ndani ya mioyo yetu. Pia alibainisha kuwa ni  fursa ya "kuchunguza pamoja njia nzuri ya maisha ambayo Mchungaji hutuongoza."

Yesu ni Mchungaji mwema

Akikumbuka kwamba katika Injili ya Yohane, Yesu anajielezea kama "Mchungaji Mwema," aliye tayari kutoa maisha yake kwa ajili ya kondoo wake, na hivyo kufichua upendo wa Mungu, Papa Leo XIV alisisitiza, "Yeye ndiye Mchungaji anayetuvuta kwake, ambaye macho yake yanaonyesha kwamba maisha ni mazuri kweli mtu anapomfuata." Papa Leo XIV alibainisha kuwa kutafakari na uhalisia wa ndani vinahitajika ili kutambua uzuri huu, akibainisha kuwa ni yule tu anayesimama, anayesikiliza, anayeomba, na kukaribisha macho ya Mchungaji anayeweza kusema kwa ujasiri, "Ninamwamini; maisha pamoja naye yanaweza kuwa mazuri kweli." "Kilicho cha ajabu zaidi," Papa Leo alibainisha, "ni kwamba, katika kuwa mwanafunzi Wake, mtu anakuwa 'mzuri' kweli; Uzuri wake hutubadilisha." Alikumbuka kwamba Mtakatifu Agostino alikuwa na uzoefu huu wa maisha, imani, na maana. Akitambua dhambi na makosa ya ujana wake, Agostino aligundua uzuri wa nuru ya kimungu inayomwongoza gizani. Uhusiano kama huo unaotegemea sala na ukimya, Papa Leo XIV alisisitiza , unapokuzwa, hutufungua kupokea na kujibu kikamilifu zawadi ya wito.

Papa anatoa mwaliko wa kuunda mazingira yanayoruhusu

Papa alisema kamwe si kulazimishwa au mfano wa ukuu mmoja unaolingana na wote ambao mtu hufuata tu" bali "matukio ya upendo na furaha. Kwa hivyo, kwa msingi wa kujali maisha ya ndani, lazima tuanze huduma yetu ya ufundi haraka na kufufua kujitolea kwetu kwa uinjilishaji. Kwa kuzingatia hilo Baba Mtakatifu aliwaalika wote, "familia, parokia, na jumuiya za kitawa , pamoja na maaskofu, mapadre  mashemasi, makatekista, waelimishaji, na waamini wote," kujitolea kikamilifu zaidi katika kuunda mazingira ambayo yanaruhusu zawadi hii kukumbatiwa, kulishwa, kulindwa, na kusindikizana nayo ili iweze kuzaa matunda mengi.

Ni wakati tu mazingira yetu yanapoangazwa na imani hai, inayodumishwa na sala ya kila mara na kutajirishwa na usindikizaji wa kidugu, ndipo wito wa Mungu unaweza kuchanua na kukomaa. Bwana anatujua sana, amehesabu nywele za vichwa vyetu, na amemtazamia kila mtu njia ya kipekee ya utakatifu na huduma," Baba Mtakatifu alisema. Lakini ufahamu huu,  lazima uwe wa pande zote mbili, kwani "tumealikwa kumjua Mungu kupitia sala, kusikiliza Neno, Sakramenti, maisha ya Kanisa na matendo ya upendo kwa kaka na dada zetu."

Kuwa na muda wa kuabudu Ekaristi

Baba Mtakatifu aliwasihi   vijana kusikiliza sauti ya Bwana, ambaye anawaalika kwenye maisha kamili na yenye matunda, akiwataka kutumia vipaji vyao na kuunganisha mapungufu na udhaifu wao na Msalaba mtukufu wa Kristo. Ili vijana wamjue Bwana, aliwahimiza kutenga muda wa kuabudu Ekaristi; Bwana, anatujua na kuangaza mioyo yetu kwa macho yake ya upendo. Kiukweli, alisisitiza, kila wito huanza na ufahamu na uzoefu wa Mungu ambaye ni upendo. Kutafakari kwa uaminifu Neno la Mungu, ili waweze kulitekeleza kila siku; na kushiriki kikamilifu katika maisha ya sakramenti na ya kikanisa ya Kanisa. Kupitia urafiki wa karibu na Yesu, Papa alisema, watagundua jinsi ya kujitoa wenyewe, iwe kupitia ndoa, ukuhani, ushemasi wa kudumu, au maisha yaliyowekwa wakfu.

Kila wito ni zawadi isiyopimika ya Kanisa 

Kila wito, ni zawadi isiyopimika kwa Kanisa na kwa wale wanaoupokea kwa furaha. Papa Leo alibainisha kuwa kumjua Bwana kunamaanisha zaidi ya yote kujifunza kujikabidhi kwake na kwa majaliwa yake, na kwamba maisha yanajifunua kama kitendo endelevu cha kumwamini Bwana na kujiachia kwake, "hata wakati mipango yake inapoharibu yetu wenyewe. Kwa njia maalum, alimtaja Mtakatifu Yosefu, ambaye, licha ya mimba ya ajabu na isiyotarajiwa ya Bikira, aliamini ujumbe wa kimungu uliofunuliwa katika ndoto na akamkaribisha Maria na mtoto wake kwa moyo mtiifu.

Mfano wa imani wa Mtakatifu Yosefu

Yosefu wa Nazareti,ni  mfano wa imani kamili katika mipango ya Mungu. Aliamini hata wakati kila kitu kilichomzunguka kilionekana kufunikwa na giza na kutokuwa na uhakika, wakati matukio yalionekana kutofautiana na mipango yake mwenyewe. Alimwamini na kujiachilia kwa Mungu. Papa alisisitiza kwamba Bwana hatuachi katika saa zetu za giza zaidi, bali anakuja kuondoa kila kivuli kwa nuru yake. Kupitia nuru na nguvu ya Roho wake, hata katikati ya majaribu na migogoro, Papa Leo alisema, tunaweza kuona wito wetu ukikua na kukomaa, tukiakisi kikamilifu uzuri wa Yule aliyetuita, uzuri ulioumbwa na uaminifu na uaminifu, licha ya majeraha na kushindwa kwetu."

Wito ni mchakato wa nguvu wa kukomaa unaondelea kuwa na urafiki na Bwana

Papa kadhalika alisema kwamba wito si sehemu isiyobadilika, bali ni mchakato wa nguvu wa kukomaa unaoendelezwa na urafiki wa karibu na Bwana wetu. Tunapaswa kuwa pamoja na Yesu, Papa alisema, tukimruhusu Roho Mtakatifu kutenda katika mioyo yetu na katika hali za maisha, na kutafsiri upya kila kitu kulingana na karama hii. Kama mzabibu na matawi," Papa alisema, maisha yetu yote lazima yajikite katika kifungo imara na muhimu na Bwana, ili tuweze kuitikia wito wake kwa moyo wote kupitia majaribu yetu. Kwa hivyo, wito,  si miliki ya papo hapo, kitu 'kilichotolewa' mara moja na kwa wote, bali ni njia inayojitokeza kama maisha yenyewe. Zawadi tuliyopokea haipaswi kulindwa tu bali pia kulishwa na uhusiano wa kila siku na Mungu ili kukua na kuzaa matunda.

Kukuza uhusiano binafsi na Mungu kupitia sala

Kwa hivyo, Papa alitoa wito kwa kila mtu kukuza uhusiano wake binafsi na Mungu kupitia sala ya kila siku na kutafakari Neno. Simama, sikiliza, na ujiamini," alisema. "Kwa njia hii, zawadi ya wito wako itakomaa, ikikuletea furaha na kutoa matunda mengi kwa Kanisa na ulimwengu." Hatimaye, katika ujumbe huo Papa  Leo XIV akimwomba  Bikira Maria, mfano wa kukubalika kwa ndani kwa zawadi za kimungu na mtaalamu wa kusikiliza kwa maombi, "aandamane nawe kila wakati katika safari hii!"

PAPA KUOMBEA MIITO 2026

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku:Just click here.

25 Machi 2026, 13:07