Tafuta

2026.03.11 Udienza Generale

Papa Leo XIV kwa EDC:Kuzingatia ukuaji wa watu na si faida tu!

Katika ujumbe uliosainiwa na Kardinali Parolin,Katibu Mkuu wa Vatican ulioelekezwa kwa Harakati ya Wajasiriamali Wakristo na Viongozi katika hafla ya kuadhimisha miaka mia moja,anabainisha kuwa Wajasiriamali wanapaswa kukuza maendeleo ya binadamu kwa heshima ya uumbaji.Papa alipendekeza kwamba:uchumi usionekane kama njia ya kukusanya faida tu,bali kama jukumu la ustawi wa jamii.Ni muhimu ulimwengu wa biashara ukatoa uaminifu,kazi thabiti na fursa kwa vijana."

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu  Leo XIV alitume ujumbe wake kwa lugha ya Kifaransa uliosainiwa na Katibu Mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, kwa Harakati ya Wajasiriamali na Viongozi Wakristo (EDC), iliyokusanyika huko Lyon, nchini Ufaransa, wakati wa kuadhimisha miaka mia moja ya harakati hiyo. Katika ujumbe huo alibainisha kwamba, "Katika enzi iliyojaa mabadiliko makubwa na udhaifu mkubwa wa kijamii," mchango wa imani ya Kikristo ni wa msingi.” Katika maandishi hayo Papa anasisitiza  akifafanua Harakati yake  kama moja ya ukaribu wa kiroho. Wakati wa kuishi katika ulimwengu wa uchumi na biashara, imani huzalisha uwajibikaji, ubunifu, na heshima kwa utu wa binadamu. Changamoto za kazi, amani, haki ya kijamii, na ulinzi wa uumbaji zimeunganishwa kwa karibu na zinahitaji mtazamo unaoweza kufahamu umoja wao ili kuongoza na kufanya uchaguzi halisi wa kibinadamu, alibainisha.

Wasifu wa Kiongozi Mkristo:hawezi kufuatilia lengo la faifa rahisi

Kutoka na na dhana hizo, Papa Leo XIV alionesha wasifu wa "kiongozi Mkristo," ambaye, ingawa anafanya kazi "ndani ya mienendo halali ya soko," hawezi kuwa na lengo lake "kufuatilia faida rahisi" au "usimamizi wa rasilimali" tu, bali lazima aelewe maendeleo ya kiuchumi kama "jamii ya watu walioitwa kukua pamoja," kama Papa Leo XIII alivyosisitiza katika hati ya mwanzilishi wa mafundisho ya kijamii ya Kanisa. “Harakati yenu, iliyozaliwa na kuendelezwa katika roho ya kiekumene, inashuhudia jinsi Injili inavyoweza kuwa chachu ya umoja na upatanisho, hata katika ulimwengu wa kiuchumi.” Ni katika mtazamo huo ambapo mafundisho ya waraka wa Kitume wa  Rerum Novarum unafaa, ambao unawaalika “wajasiriamali kuheshimu utu wa kila mfanyakazi na kuwalinda walio hatarini zaidi.” Jukumu la kijamii la biashara, Papa Leo XIV alisisitiza zaidi, kwa hivyo “haliwezi kutafsiriwa tu kwa maneno ya kiuchumi, kama chombo cha uzalishaji au mkusanyiko, lakini kwa upande wa uwezo wake wa kukuza kile kilicho cha kibinadamu, kuimarisha vifungo vya jamii, na kuheshimu kazi ya  uumbaji."

Viongozi wa Kikristo wanaitwa kukuza uchumi unaochanganya ufanisi na ubinadamu hasa vijana

Papa Leo XIV  katika  ujumbe huo aidha alielekeza mawazo yake kwenye “nafasi ya vizazi vipya katika soko la ajira. Uchumi unaomwilishwa na imani ya Kikristo huwapatia ujasiri na huwapatia fursa, kazi thabiti, kama kitendo cha uwajibikaji na matumaini kinachoweza kuzuia kutengwa na kutengwa.  Kwa  njia hiyo, viongozi wa Kikristo wanaitwa kukuza uchumi unaochanganya ufanisi na ubinadamu, kuwapa vijana sio kazi tu, bali pia njia za ukuaji, elimu, na ushiriki wenye uwajibikaji, unaoweza kuzalisha maendeleo halisi ya kibinadamu. Mwishoni mwa ujumbe wake, Papa  Leo XIV anarudia "shukrani" yake kwa kazi ya Harakati ya Wajasiriamali na Viongozi Wakristo na kuwatia moyo wanachama wake kuendelea na "safari yao" na kujenga Ufalme wa Mungu kila siku, kama "sehemu muhimu ya jumuiya ya Kanisa."

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku bonyeza hapa: Just click here.

13 Machi 2026, 15:00