Tafuta

2026.03.28 Zafari ya kurudi kutoka Monaco.Kabla ya kuanza safari aliagwa na wenyeji wake, Wafalme wa Monaco. 2026.03.28 Zafari ya kurudi kutoka Monaco.Kabla ya kuanza safari aliagwa na wenyeji wake, Wafalme wa Monaco.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV aaga Ufalme wa Monaco na kurudi Roma

Saa 11:30 jioni,safari ya Helikopta ilianza na baada ya takriban saa mbili,Papa atatua kwenye Uwanja wa Helikopta wa Vatican.Kabla ya kuondoka,aliwasalimu Mfalme Albert II na Mkewe Charlene,ambao,katika telegramu,yake aliwashukuru kwa makaribisho ya joto.

Vatican News

Helikopta iliyombeba Baba Mtakatifu Leo XIV ilianza  safari yapata saa 11:25 jioni hivi. Zaidi ya saa nane baada ya kuwasili kwake, asubuhi ya Jumamosi tarehe 28 Machi 2026, Baba Mtakatifu alihitimisha Ziara yake ya Kitume ya kwenda Ufalme wa Monaco, ikiwa ni ziara yake ya pili ya Upapa kuwa nje ya nchi na ya kwanza barani Ulaya.

Papa akisindikizwa na wenyeji wake
Papa akisindikizwa na wenyeji wake   (@Vatican Media)

Hafla ya kuaga ilifanyika kwenye Uwanja wa Helikopta wa Monaco, kwenye mandhari nzuri ya bahari. Baada ya kuwasalimu wenyeji wake na ujumbe wa Monaco katika ukumbi, Papa Leo XIV alipitia Walinzi wa Heshima na kuwaaga: Mfalme Albert II na Malkia Charlene. Mazungumzo mafupi yalifanyika kati yao, ikifuatiwa na salamu na shukrani kwa makaribisho waliyopokea.

Papa akiagwa na wenyeji wake Wafalme wa Monaco
Papa akiagwa na wenyeji wake Wafalme wa Monaco   (@Vatican Media)

Kisha Papa Leo XIV alipanda helikopta. Ndege ilipaa kutoka ardhi ya Monaco yapata saa 11:30 jioni na ndani ya dakika chache ilikuwa iko juu ya usawa wa Bahari. Katika telegramu iliyotumwa kwa Mfalme Albert II, Papa Leo XIV alitoa shukrani zake za dhati kwa Mfalme, familia ya kifalme, serikali, na watu wote wa Monaco: "kwa mapokezi ya joto na ukarimu" uliotolewa wakati wa ziara yake ya kitume. "Ninaomba, kwamba Mungu Mwenyezi awabariki nyote kwa amani na nguvu," aliandika Papa  na kuhitimisha kwa kuwapatia baraka zake. Helikopta aliyopanda ilitarajiwa kutua kwenye Uwanja wa Herikopta wa Vatican takriban masaa mawili ya safari.

Kwa njia hiyo Papa baada ya kuaga Ufalme huo, alisafiri na Helikopta iliyotua kwenye Uwanja wa Helikopta wa Vatican yapata saa 1:00 usiku, masaa ya Ulaya.

Habari hii imesasishwa saa 3.31 usiku, saa za Ulaya.

Safari ya kurudi kutoka Monaco
Safari ya kurudi kutoka Monaco   (@Vatican Media)
PAPA KUFIKA ROMA

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku:Just click here.

28 Machi 2026, 19:10