Tafuta

2025.12.31 Papa alikutana na wasemimnari na vijana mapadre wa majimbo wa Harakati ya Wafocolari huko (Castel Gandolfo, 29 dicembre 2025). 2025.12.31 Papa alikutana na wasemimnari na vijana mapadre wa majimbo wa Harakati ya Wafocolari huko (Castel Gandolfo, 29 dicembre 2025). 

Papa kwa mapadre na waseminari Wafocolari:Kuweni mashuhuda wa matumaini

Papa Leo XIV akiwa katika katekesi yake aliwasalimia katika Uwanja wa Mtakatifu Petro kundi la Waseminari na Mapadre wa Harakati ya Wafocolari iliyoanzishwa na Chiara Lubich,ambao alikutana nao huko Castel Gandolfo tarehe 29 Desemba 2025.

Vatican News

Wakati mara mbili pamoja na Papa, mawasiliano ya moja kwa moja na kisha kama wapokeaji wa salamu iliyopokelewa kutoka katika umati kwenye Uwanja wa Mtakatifu Petro. Huu ulikuwa uzoefu wa waseminari 35 na mapadre vijana wa majimbo  kutoka nchi 18 na mabara manne, wanachama wa Harakati ya Wafocolari, walioshiriki katika mkutano huko Castel Gandolfo kuanzia Desemba 26 hadi 30 kuhusu mada ya "Kuishi Ukaribu," iliyoongozwa na maneno Papa Leo XIV aliyowaandikia waseminari wakati wa Jubilei kuwa: "Leo, katika muktadha wa kijamii na kiutamaduni uliojaa migogoro na kujipenda, tunahitaji kujifunza kupenda na kufanya hivyo kama Yesu."

Papa akutana na wanachama wafocolari( Mapadre na waseminari)
Papa akutana na wanachama wafocolari( Mapadre na waseminari)

Mwaliko wa Papa

Mnamo tarehe 29 Desemba 2025 akiwa huku Castel Gandolfo, kama kawaida anavyofanya kati ya Jumatatu na Jumanne za majuma haya, Papa mwenyewe aliwakaribisha nyumbani kwake ili kusalimiano na kila mmoja wao kuwa kupenana mikono na kuwatia moyo katika huduma ambayo wamejiweka wakfu au wanajiandaa kufanya hivyo.

Papa akutana na wanachama Aafocolari( Mapadre na Waseminari)
Papa akutana na wanachama Aafocolari( Mapadre na Waseminari)

Akithamini fursa ya uwepo wao huko Roma kwa ajili ya hija mwishoni mwa Jubilei, Papa Leo XIV aliwaalika "kutafuta zawadi ya matumaini" na kuwa mashahidi wake "mtakaporudi katika nchi zenu za asili." Hata baada ya Sala ya Bwana Dominika tarehe 28 Desemba 2025, Papa alirudia kueleza kuwa: "Sote tutembee pamoja, tukijitahidi kuwa mashahidi na tumaini kila siku."

Kongamano

Wakati wa Kongamano, mawasilisho na ushuhuda vilishughulikia changamoto za maisha ya seminari leo, hususan mada za ukaribu na hisia, kutafsiri vipengele vya wito kwa kuzingatia karama ya umoja ambayo ndiyo msingi wa Harakati iliyoanzishwa na Chiara Lubich. Rais wa Harakati hiyo, Margaret Karram, alishirikiana na washiriki wa kongamano na kujibu maswali, akiwatia moyo waumbwe na Neno, Ekaristi, na roho ya huduma, ili wawe makuhani walio wazi kwa ushirika.

Papa alikutana na mapadre na waseminari Wafocolari
Papa alikutana na mapadre na waseminari Wafocolari   (©Masera CSC Audiovisivi)

Wakati wa kongamano, hilo kadhalika mapadre na waseminari walipata siku ya hija iliyowapeleka kwenye Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu na kwenye kaburi la Papa Francisko, kisha hhadi Mtakatifu Petro ili kushiriki ksala  Malaika wa Bwana na hivyo Jumatano tarehe 31 Desemba 2025  wakashiriki Katekesi ya  mwisho ya mwaka na Papa Leo XIV.

Papa na wafokolari mapadre

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here

01 Januari 2026, 10:00