Tafuta

2025.11.03 Katika Kanisa Kuu  Bikira Maria Mkuu: Papa Leo alisali mbelel ya Kaburi ya Papa Francisko. Santa Maria Maggiore - Preghiera davanti alla Tomba di Papa Francesco 2025.11.03 Katika Kanisa Kuu Bikira Maria Mkuu: Papa Leo alisali mbelel ya Kaburi ya Papa Francisko. Santa Maria Maggiore - Preghiera davanti alla Tomba di Papa Francesco  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV asali katika Kaburi la Hayati Papa Francisko

Kabla ya kuelekea Castel Gandolfo kwa siku yake ya kawaida ya kupumzika kila Juma,Baba Mtakatifu Leo XIV aliingia karibu saa 2:05 za usiku,masaa ya Ulaya katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu ili kusali mbele ya kaburi la Papa Francisko.

Na Salvatore Cernuzio - Vatican.

Kabla ya kuelekea Castel Gandolfo kwa siku yake ya kawaida ya kupumzika kila Juma, Baba Mtakatifu Leo XIV aliingia karibu saa 2:05 za Usiku, masaa ya Ulaya katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu ili kusali mbele ya kaburi la Papa Francisko.

Kwenye bamba la marumaru ambapo huwekwa waridi jeupe ambalo wanaweka kila mara katika kumbukumbu ya Mtakatifu Thérèse wa Lisieux, la uwepo wa kiroho wa kudumu katika maisha ya Papa wa Argentina ma hivyo Papa Leo  XIV naye aliweka shada la waridi jeupe. Ilikuwa ishara ya heshima kwa mtangulizi wake, aliyezikwa kati ya Kikanisa cha Sforza na Kikanisa cha Pauline. Kikanisa cha mwisho ni nyumbani kwa Picha ya Salus Populi Romani, (yaani Afya ya Watu wa Roma) ambayo mara nyingi ilitembelewa na Papa Francis kabla na baada ya kila safari ya kimataifa au kulazwa hospitalini.

Papa Leo mbele ya Kaburi la Papa Francisko kuweka waridi na kusali
Papa Leo mbele ya Kaburi la Papa Francisko kuweka waridi na kusali   (@Vatican Media)

Kulingana na Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican, Papa Leo XIV, pia alisimama kwa sala mbele ya Picha ya Maria kabla ya kuondoka kwenye Kanisa kuu karibu saa 2:15 usiku na kuendelea na safari yake kwenda Castel Gandolfo.

Pope Leo at the tomb of his predecessor

Pope Leo katika kaburi la Mtangulizi wake  

Misa ya kumwombea kwa Papa Francisko


Mapema siku hiyo Novemba 3, Papa Leo XIV alikuwa ameadhimisha Misa katika Madhabahu ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwa kuombea roho za Marehemu kwa ajili ya Papa Francisko na makardinali na maaskofu waliofariki mwaka 2025. Kwa "upendo mkubwa," Baba Mtakatifu aliitoa Misa hiyo kwa ajili ya mtangulizi wake, ambaye, alikumbuka katika mahubiri yake, kwamba "alikufa baada ya kufungua Mlango Mtakatifu na kutoa Baraka ya Pasaka kwa Roma na Ulimwengu wote. Shukrani kwa Jubilei, adhimisho hili kwangu kwa mara  ya kwanza, linachukua maana maalum: lina ladha ya tumaini la Kikristo."

Pope Leo prays in front of the image of Salus Populi Romani

Papa Leo akisali mbele ya Picha Salus Populi Romani

Tumaini hili, Papa Leo XIV aliongeza baadaye katika tafakari yake, lilikuwa moja ambalo Papa Francisko na maaskofu wengine waliokufa katika miezi ya hivi karibuni "waliishi, walishuhudia, na kufundisha."

Ziara za awali kwenye kaburi katika Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu

Mnamo tarehe 10 Mei, siku mbili tu baada ya kuchaguliwa kwake katika  Kiti cha  Mtume Petro, Papa Leo alitembelea kaburi la Papa wa Argentina, ambalo hutembelewa kila siku na waamini na mahujaji wengi. Alasiri hiyo, Papa aliyechaguliwa hivi karibuni aliweka maua kwenye kaburi na kusimama kwa muda mfupi katika maombi. Alifanya vivyo hivyo tena tarehe 22 Juni, kufuatia maandamano ya Sherehe ya Mwili na Damu ya Kristo, kutoka Mtakatifu Yohane Lateran hadi Basilika ya Mtakatifu Maria  Mkuu.

Papa kwa Maria Mkuu

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku kwa kubonyeza hapa: Just click here

04 Novemba 2025, 09:10