Tafuta

2025.10.06 Bwana  Gitanas Nauseda, Rais wa Jamhuri ya Lithuania. 2025.10.06 Bwana Gitanas Nauseda, Rais wa Jamhuri ya Lithuania.  (@Vatican Media)

Vatican:Papa akutana na Rais wa Jamhuri wa Lithuania

Papa Leo XIV,Oktoba 6 alikutana na Bwana Gitanas Nausėda mjini Vatican, Rais wa Jamhuri ya Lithuania.Katika mijadala iliyofuata katika Sekretarieti ya Vatican,uhusiano mzuri kati ya nchi ya Lithuania na Vatican ulithibitishwa tena pamoja na hitaji la kufufua diplomasia ili kumaliza mzozo wa Ukraine.

Vatican News

Jumatatu tarehe 6 Oktoba 2025, Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana katika Jumba la Kitume mjini Vatican, Rais wa Jamhuri wa Lithuania, Bwana Gitanas Nausėda, na baadaye alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican akisindikizana na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirikia ya Kimataifa.

Papa na Rais wa Lithuania
Papa na Rais wa Lithuania   (@Vatican Media)

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi za vyombo vya habari Vatican, imebainisha kuwa “wakati wa mazungumzo mazuri, kati ya Sekretarieti ya Vatican walielezea, kupendezwa mahusiano mazuri yenye matunda ambayo yapo kati ya Vatican na Jamhuri ya Lithuania.

Wakati wa kubadilishana zawadi
Wakati wa kubadilishana zawadi   (@Vatican Media)

Katika “mazungumzo hayo aidha walisisitiza juu ya baadhi ya matatizo zenye tabia ya Kimataifa, kwa namna ya pekee yanayohusu vita nchini Ukraine, wameelezea ulazima wa kina wa kutafuta suluhisho ya kidiplomasia, kwenda mbali zaidi ya hatari zinazopanuka za migogoro zisizo tegemewa na matokeo yasiyoelezeka.”

Picha ya Rais wa Lithuania na kikundi kizima alichoambatana nacho
Picha ya Rais wa Lithuania na kikundi kizima alichoambatana nacho   (@Vatican Media)
Papa na Rais wa Lithuania

Asante sana kusoma makala hii, ikiwa unakata kubaki na masasisho zaidi, tunakualika kujiandikisha hapa: Just click here

06 Oktoba 2025, 17:40