Tafuta

2025.09.18   Kutangazwa rasmi kwa Monsinyo Wachowski kama Balozi wa Vatican nchini Iraq. 2025.09.18 Kutangazwa rasmi kwa Monsinyo Wachowski kama Balozi wa Vatican nchini Iraq. 

Papa amteua Balozi mpya wa Iraq,Monsinyo Wachowski

Katika huduma ya kidiplomasia ya Kiti Kitakatifu tangu 2004,ambaye hapo awali alikuwa katibu Msaidizi wa Mahusiano na Mataifa,Papa alimpandisha hadhi kwenye kiti cha heshima cha Villamagna di Proconsolare, akiwa na hadhi ya Askofu mkuu na Balozi mpya wa Iraq.

Vatican News

Baba Mtakatifu  Leo XIV alimteua tarehe 18 Septemba  2025, Monsinyo Mirosław Stanisław Wachowski, ambaye hadi uteuzi wake alikuwa ni  Katibu Msaidizi wa Mahusiano na Mataifa, kuwa Balozi mpya wa Vatican  nchini Iraq, na wakati huo huo akimpandisha hadi kwenye kiti cha heshima cha Villamagna di Proconsolare, akiwa na hadhi ya Askofu Mkuu. Tangazo la uteuzi huo limetolewa  asubuhi  ya Alhamisi na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa  Vatican wa Mahusiano na Mataifa, na Mashirikia ya Kimataifa mbele ya wahusika wa kitengo cha  tatu cha Sekretarieti ya Vatican.

Alizaliwa wa Pisz, Poland, tarehe 8 Mei  1970.  Monsinyo Wachowski alipewa Daraja Takatifu la Upadre mnamo 15 Juni 1996, kwa ajili ya  Jimbo la Ełk. Ana shahada ya Sheria ya Kanoni.

Aliingia katika huduma ya kidiplomasia ya Kiti Kitakatifu,  tarehe 1 Julai  2004 na kuhudumu katika Uwakilishi wa Kipapa nchini Senegal, Utume wa Kudumu kwa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA), Shirika la Usalama na Ushirikiano Barani Ulaya(OSCE); Ofisi ya Umoja wa Mataifa na Mashirika Maalum huko Vienna, Ofisi ya Ubalozi wa Vatican  huko Poland, na hivi karibuni katika Kitengo cha Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa ya Sekretarieti ya Vatican. Aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Mahusiano na Mataifa mnamo tarehe 24 Oktoba 24. Anajua kuzungumza Kiitaliano, Kiingereza, Kifaransa, Kihispania na Kirusi kwa ufasaha.

18 Septemba 2025, 18:30