Tafuta

2025.09.29 Papa alimutana naMrithi wa Mfalme Salman bin Hamad Al Khalifa, na Waziri Mkuu wa Ufalme wa Bahrein. 2025.09.29 Papa alimutana naMrithi wa Mfalme Salman bin Hamad Al Khalifa, na Waziri Mkuu wa Ufalme wa Bahrein.  (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Mwana Mfalme na Wazir Mkuu wa Ufalme wa Bahrein

Wakati wa mazungumzo yao Septemba 29 mjini Vatican na Sekretarieti ya Vatican,walionesha uwepo wa mahusiano mazuri na ya sehemu zote mbili. Viongozi hao walitazama kuhusu siasa za Ufalme wa Bahrein katika kuhamasisha mazunguzmo ya kidini na uwepo wa amani kati ya dini tofauti katika Ufalme huo.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV, Jumatatu tarehe 29 Septemba 2025 alikutana katika Jumba la Kitume mjini Vatican na Mwana Mfalme na Waziri Mkuu wa Ufalme wa  Bahrein, Salman bin Hamad Al Khalifa, ambaye baadaye alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, akisindikizana na Monsinyo Mirosław Stanisław Wachowski.

Mwana Mfalme na Ujumbe wake katika picha ya pamoja
Mwana Mfalme na Ujumbe wake katika picha ya pamoja   (@VATICAN MEDIA)

“Wakati wa majadiliano ya kina,kuridhika kulioneshwa kwa uhusiano mzuri baina ya nchi mbili, na makubaliano yalifikiwa juu ya hamu ya kuimarisha zaidi. Kisha majadiliano yalilenga sera ya Ufalme wa Bahrain ya kukuza mazungumzo ya kidini na kuishi pamoja kwa amani kati ya dini tofauti katika Ufalme, kwa kujitolea kwa amani kati ya mataifa." Hayo yalithibitishwa na  Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican.

29 Septemba 2025, 15:36